• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII 872 KUPATIKANA RUANGWA

Posted on: July 9th, 2024

Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa Kushirikiana na Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetoa nafasi 872 kwa wananchi watakaowania nafasi ya Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi ambao watatambuliwa kupitia Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya ngazi ya jamii.


Akizungumza katika Kikao na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ruangwa leo tarehe 9, 2024 katika Ofisi ya Mkurugenzi, Afisa Mpango wa Taifa wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii Bi.Orsolina Tolage kutoka Wizara ya Afya, Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma amesema kila kitongoji kutakuwa na Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wawili.


"Katika kuhakikisha huduma za Afya zinakuwa karibu zaidi na wananchi Serikali imejipanga ambapo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa tunatarajia kupata Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii 872, wawiliwawili kila kitongoji jinsi ya kiume mmoja na jinsi ya kike mmoja , hivyo wataomba nafasi na watachaguliwa kupitia mikutano ya kijiji au mtaa"amesema.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Frank Chonya ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweka kipaumbele suala la Afya hasa kwa kuweka Mkakati wa kuwa na Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii katika kata 22, vijiji 90 na vitongoji 436 katika Halmashauri hiyo.


"Naishukuru Serikali kwa kuimarisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na hili suala la Mpango Jumuishi wa Wahudumu Ngazi ya Jamii limekuja katika muda mwafaka hivyo tutashirikiana kuhakikisha uchaguzi wa CHW's unafanyika kwa ufasaha.


Ikumbukwe kuwa Uchaguzi wa kuwachagua Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii katika Halmashauri ya Ruangwa unatarajia kuanza mwezi huu ikiwa ni katika Utekelezaji wa Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii Uliozinduliwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango tarehe 31,Januari,2024 na lengo ni kupata Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wapatao 137,294 katika Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa