HAYA NDIYO MADINI YANAYOPATIKANA WILAYA YA RUANGWA
1. Graphite (Bunyu)
Yanapatikana katika vijiji vya Mihewe, Mtondo, Nambilanje, Matambarale, Nangurugai, Nachiungo, Namakuku, Namkonjera, na Chunyu.
Matumizi: Graphite hutumika kutengeneza betri, penseli, vifaa vya elektroniki, na pia katika sekta ya magari ya umeme.
2. Dhahabu na Shaba
Yanachimbwa katika vijiji vya Namungo, Nangurugai, Mihewe, Nambilanje, Kitandi, na Nkowe.
Matumizi: Dhahabu hutumika kutengeneza mapambo, kuhifadhi thamani (akiba), na katika sekta ya elektroniki. Shaba hutumika kwa ajili ya nyaya za umeme, mabomba na vifaa vya majumbani.
3. Madini ya Vito
Blue Sapphire: Inapatikana Nangurugai na Nachiungo.
Red Garnet na Green Garnet: Zipo Namungo, Chunyu, na Mihewe.
Greenstones (Chrysalises & Greentourmaline): Zipo Namungo, Nandagala, na Mihewe.
Matumizi: Madini haya hutumika zaidi kutengeneza vito vya mapambo, pete, hereni, mikufu na pia huingizwa kwenye sekta ya mitindo na bidhaa za kifahari.
4. White Marble
Yanapatikana katika vijiji vya Mihewe, Namkonjera, na Nanjaru.
Matumizi: White marble hutumika katika ujenzi wa majengo ya kifahari, mapambo ya ndani (interior design), sakafu, meza, na vigae vya ukutani.
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa