• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

Posted on: November 18th, 2025

Wanawake na vijana wa Wilaya ya Ruangwa wamepata fursa muhimu ya kuelimishwa na kuwezeshwa kupitia Kongamano la Fursa za Mikopo za Kuongeza Thamani ya Zao la Korosho, lililofanyika leo Novemba 18, 2025, katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa.


Kongamano hilo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Wilaya ya Ruangwa, NMB Foundation na Rabo Foundation, likiwa na lengo la kuwajengea wanavikundi uelewa wa uchakataji, uzalishaji wenye tija, na usimamizi wa mikopo kwa maendeleo ya kiuchumi.

Akifungua kongamano hilo, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, aliweka msisitizo mkubwa katika kuongeza thamani ya korosho kama njia ya kuongeza pato la taifa na kuimarisha uchumi wa kaya.


Amesema mazao yanayozalishwa lazima yaongezwe thamani ili wakulima wanufaike zaidi, akibainisha kuwa mlolongo wa thamani wa korosho umeendelea kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi wa Wilaya na taifa kwa ujumla.


“Mazao yote yanayozalishwa yanapaswa kuongezwa thamani ili wananchi wanufaike zaidi na jasho lao. Uzalishaji hauwezi kukua bila kushirikiana na wadau kama NMB; tunawapongeza kwa kuisaidia serikali kuimarisha uchakataji wa zao la korosho,” amesema Mhe. Ngoma.

Mhe. Ngoma aliwashukuru NMB Foundation pamoja na Rabo Foundation kwa kuwekeza katika mifumo ya uchakataji na utoaji wa mikopo rafiki kwa vikundi vya wanawake na vijana, huku akisisitiza kuwa uzalishaji hauwezi kukua bila ushirikiano wa wadau. Aliwataka wananchi kutumia fursa hizo za mikopo vizuri kwa kuimarisha uzalishaji na biashara zao.


Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndg. Rashid Namkulala, aliishukuru NMB kupitia NMB Foundation kwa ushirikiano wao wa karibu na Serikali, ambao umewawezesha wakulima na wanavikundi wa uzalishaji wa korosho.

Alibainisha kuwa korosho ni sehemu muhimu ya pato la taifa, hivyo juhudi za kuongeza uzalishaji na ubunifu zinathaminiwa sana na Halmashauri. Aliongeza kuwa Halmashauri iko tayari kuendelea kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika kuhakikisha makundi ya wanawake na vijana yanapata ujuzi, mitaji, elimu ya fedha, mbinu za kuongeza thamani ya mazao, pamoja na mikopo na mafunzo yanayotolewa ili kuongeza uwezo wa wanavikundi kusimamia miradi kwa weledi na kuongeza ushiriki wao katika uchumi wa Wilaya.


Katika kongamano hilo, wanavikundi walipata mafunzo kuhusu namna ya kuongeza thamani ya korosho kupitia uchakataji, uongezaji ubora, upatikanaji wa masoko, pamoja na utunzaji bora wa fedha. Mafunzo hayo yamelenga kuhakikisha rasilimali hizo zinabadilishwa kuwa bidhaa zenye ushindani ndani na nje ya nchi.

Viongozi na wadau hao walisema kuwa fursa za mikopo na mafunzo kwa wanawake na vijana ni muhimu kwa kujenga kizazi kinachojitegemea kiuchumi na kuongeza mchango wa Ruangwa katika uzalishaji wa korosho nchini. Waliwataka wanavikundi kuendelea kuungana, kushirikiana, na kutumia maarifa waliyopewa ili kuongeza tija na kuimarisha maendeleo ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA YAPATA USAJILI KWA MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA (CPD)

    November 20, 2025
  • MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

    November 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE KITAIFA 2025

    November 15, 2025
  • MAAFISA UTAMADUNI WAKUTANA NA WALAMBO, NGARIBA NA WAMILIKI WA VIWANJA VYA JANDO NA UNYAGO

    November 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa