• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Tehama



                                                                                                  Kaimu Mkuu wa Kitengo Cha Tehama

Ndg: Jitetee Mbonde



 HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA

(Barua zote zitumwe kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa)



OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI (W),
S.L.P 51,

RUANGWA





Simu: 0732 933 212
Fax: 0732 933 259
 


_____________ ______

TAARIFA YA KITENGO CHA TEHAMA

1.0 UTANGULIZI Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ni moja ya vitengo vilivyoanzishwa na serikali mwaka 2012 kikiwa na lengo la kusimamia masuala ya mifumo ya teknolojia, usambazaji wa habari na kuimarisha mahusiano ya taasisi za umma na taasisi zingine.

Teknolojia imelenga zaidi kuhakikisha inasimamia mifumo inayowekwa na serikali ambapo kwasasa serikali inafunga mifumo mbalimbali ya kidigitali kwa kushirikiana na taasis ya kiserikali ya serikali mtandao (egovernment) ili kuhakikisha taarifa zote za fedha na zingine zinapatikana kwa njia ya mitandao yenye mifumo maalum ya kidigitali. Na kuachana na mazoea ya zamani ya kutumia risiti za kuandika kwa mkono.

Habari imelenga katika kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi kuhusu mambo yanayoendelea katika taasis husika kwa wakati ikiwemo takwimu mbalimbali ili kuwaweka karibu zaidi wananchi na taasis yao lakini pia kuwapasha mambo mbalimbali yanayotekelezwa

Simu: +255 732 933 212

Nukushi: +255 732 933 259

Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz 

Tovuti: www.ruangwadc.go.tz

Mkurugenzi Mtendaji(W)

S.L.P 51, 

RUANGWA. 

na serikali ikiwa ni pamoja yanayotarajiwa kutekelezwa na serikali kwa kutumia njia zote ikiwemo vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na tovuti.

Mahusiano imelenga katika kuimarisha mahusiano ya idara moja na nyingine katika taasis husika, taasis na taasis nyingine na taasis na wananchi ili kuhakikisha kuna maelewano mazuri na kufanya kazi kwa pamoja ili kuleta picha chanya ya maendeleo katika taasis husika.

2.0 MAWASILIANO YA WATUMISHI WA IDARA AU KITENGO

Kitengo hiki kina watumishi watatu kwasasa ambao ni

(1)Jitete Mbonde                Mkuu wa kitengo 

(2)Mwanakheri Ahmed        Afisa Habari

(3)David Mapunda            Fundi sanifu daraja I

 

3.0. KAZI ZA IDARA

Kitengo cha TEHAMA kinafanya kazi mbalimbali ambapo zimegawanyika kama ifuatavyo

3.1 MAJUKUMU YA AFISA TEHAMA

1. Kuangalia mwenendo wa utendaji kazi wa mfumo wa TEHAMA

2. Kutoa nakala ngumu na laini ya ripoti mbalimbali kutoka kwenye mifumo ya TEHAMA.

3. Kuhifadhi taarifa zinazoingizwa kwenye program tumizi.

4. Kutunza kumbukumbu za kazi zilizofanyika katika programu tumizi.

5. Kusahihisha makosa yanayotokea katika taarifa zilizofanyiwa mchakato katika program za mifumo ya TEHAMA.

6. Kuandaa mahitaji ya vifaa na vipuli vya mifumo ya TEHAMA.

7. Kuandaa mpango kazi na majukumu ya kila siku.

8. Kutathmini mwenendo wa utendaji kazi wa mifumo.

9. Kufanya marekebisho ya kasoro zinazojitokeza katika mwenendo wa uingizwaji wa taarifa kwenye mifumo.

10. Kuandika ripoti ya makosa yaliyojitokeza kwenye taarifa zilizofanyiwa mchakato katika mifumo ya TEHAMA katika uingizaji wa takwimu kwenye program tumizi.

11. Kuangalia mwenendo wa usalama wa taarifa na mitambo ya TEHAMA.

12. Kutathmini na kutoa taarifa kuhusu hitilafu za mfumo wa TEHAMA.

13. Kutafsiri mwongozo wa matumizi ya mifumo na kutoa maelekezo ya namna ya kutekeleza.

14. Kuandaa na kutoa mafunzo ya namna ya kuendesha mifumo ya TEHAMA kwa operata.

15. Kusimamia mafunzo ya uendeshaji wa mifumo ya TEHAMA mahali pa kazi

16. Kubuni mbinu za utekelezaji /uboreshaji wa majukumu ya uendeshaji wa mifumo ya TEHAMA

17. Kushiriki katika mpango wa kuandaa namna bora ya uthibiti wa taarifa

18. Kufanya ukaguzi wa ubora wa vifaa vya TEHAMA na kurekebisha ipasavyo

19. Kufanya matengenezo madogomadogo ya vifaa vya TEHAMA

20. Kufanya matengenezo ya miundombinu ya TEHAMA

21. Kuchukua hatua za kiusalama kulinda vifaa vya TEHAMA

22. Kukagua na kutambua vifaa vinavyoitaji matengenezo

23. Kutoa huduma kwa watumiaji wa vifaa vya TEHAMA (Help Desk)

24. Kusimamia ukaguzi na ufungaji wa vifaa vipya vya TEHAMA

25. Kufanya ukaguzi wa ubora wa program- tumizi na mifumo ya habari

26. Kufanya marekebisho madogo madogo katika program – tumizi

27. Kutoa huduma kwa watumiaji wa program – tumizi na mifumo ya habari (Help desk)

28. Kufanya makisio ya mahitaji na gharama za vifaa na miundombinu ya TEHAMA

29. Kutunza kumbukumbu za matengenezo ya vifaa vya TEHAMA

30. Kutayarisha mpango wa matengenezo ya vifaa na miundombinu ya TEHAMA (Preventive maintenance plan)

31.Kusimamia ubora na viwango kwa vifaa vya TEHAMA vinavyonunuliwa,kufungwa na vinavyotumika

32. Kusimamia utekelezaji wa mikakati ya kuweka mifumo ya habari yenye lengo la kuongeza tija na uboreshaji wa huduma zitolewazo

33. Kusimamia utekelezaji wa miradi inayolenga uendelezaji wa serikali mtandao

34. Kutoa ushauri wa kitaalam katika usanifu na utengenezaji wa Tovuti na medi anuai

35. Kufundisha waajiriwa wapya katika matumizi ya program tumizi za kompyuta

36. Kurejesha utendaji mzuri wa mifumo ya TEHAMA panapotokea uharibifu

37.Kutekeleza mipango ya kudhibiti na kunusuru uharibifu katika mifumo ya TEHAMA (implement system and network disaster recovery and business continuity plan)

38. Kusimamia utoaji wa huduma za kitaalam za usalama wa mifumo ya TEHAMA na kuelimisha watumiaji.

3.2 MAJUKUMU YA AFISA HABARI

Afisa habari wa Wilaya ya Ruangwa pamoja na maeneo mengine wana kazi mbalimbali kama zifuatazo;

1. Kusimamia sera, mikakati na miongozo inayotolewa na Serikali Kuu juu ya uendeshaji wa kazi za habari na mahusiano;

2. Kuandaa mpango, bajeti, mpango kazi, mpango mkakati wa kuteleza kazi za habari na mahusiano katika Halmashauri;

3. Kutangaza na kuchapisha kazi na miradi inayofanyika katika Halmashauri;

4. Kutangaza maeneo ya uwekezaji ya Halmashauri katika tovuti, radio, magazeti na majarida;

5. Kuhakikisha tovuti ya Halmashauri ina taarifa mpya kila wakati pamoja na District Profile;

6. Kuandaa na kutoa majarida kuhusu Halmashauri;

7. Kushiriki katika mijadala ya jamii kuhusu masuala ya Halmashauri

8. Kutumia TEHAMA katika kutoa elimu kwa jamii;

9. Kusimamia press briefing za Halmashauri;

10. Kushauri Halmashauri juu ya uandaaji, uzalishaji na usambazaji wa nyaraka kwa wadau mbalimbali

11. Kushirikiana kwa karibu na afisa habari na uhusiano wa Mkoa na wa Wizara ili kubadilisha uzoefu na kujengeana uwezo.

12. Kuisemea Halmashauri kwa wananchi

13. Kutengeneza ,maktaba ya picha za mnato na video za halmashauri ya mji

14. Kuandaa na kushiriki maonyesho mbalimbali yanahusiana na Halmashauri kwa kutengeneza vipeperushi na makala za maonyesho husika

15. Kuhamasisha shughuli mbalimbali za Halmashauri za kitaifa na kiwilaya kwa kutumia na vyombo vya habari

4.0. HUDUMA ZITOLEWAZO KATIKA IDARA AU KITENGO

Mwananchi anaweza kupata huduma zifuatazo katika kitengo cha TEHAMA

1. Elimu ya mifumo mbalimbali iliyowekwa na serikali inavyofanyakazi

2. Ushauri wa jinsi ya kutumia mitandao ya kijamii kufikisha ujumbe

3. Kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali yanayotekelezwa na halmashauri

4. Ushauri wa jinsi ya kupata vifaa bora vya kiteknolijia na habari

5.0. MATARAJIO YA IDAYA AU KITENGO

Kitengo kinatarajia kufanya mambo mbalimbali kwa kipindi cha miaka mitano kama ifuatavyo.

1. Kutoa elimu zaidi kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutumia mifumo ya kielektroniki na faida

2. Kubuni njia za kisasa zaidi za kufikisha ujumbe kwa wananchi

3. Kufunga mifumo zaidi ya kelektroniki ili kukuza mapato ya Halmashauri

4. Kubuni njia zaidi za kuongeza usalama wa vifaa vya kielekroniki

5. Kuitangaza Halmashauri na kazi zake kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari


KARIBUNI SANA KATIKA KITENGO CHA TEHAMA




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MPARA WAFANYA USAFI KUJIANDAA NA MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa