• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

TFRA imarisheni upatikanaji wa mbolea wilaya ya ruangwa

Posted on: April 11th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ameipongeza Mamlaka ya Udhibiti Mbolea Tanzania (TFRA) Kwa kazi ya kuwaelimisha wakulima juu ya matumizi ya mbolea katika kuzalisha mazao mbalimbali, ameeleza kuwa kazi hiyo ni nzuri na yenye tija kwa Mkoa na Taifa. Pia aliwaomba  TFRA waone umuhimu wa kutafuta na kuwaweka wakulima karibu zaidi na vifaa vya kupima udongo ili iwe rahisi kwao kufahamu mazao sahihi kwa udongo walio nao pamoja na  mbolea sahihi.

Ameyasema hayo tarehe 12/04/2022 wakati wa maadhimisho ya siku ya mkulima iliyofanyika kijiji cha Chimbila B kilichopo kata ya Mnacho, maadhimisho yaliyobeba kauli mbiu ya "Tumia Mbolea kuongeza Kipato na Tija"


Mkuu wa Mkoa aliwataka  TFRA kuendelea kuwashika mkono wakulima waliopata elimu ya mtumizi bora ya mbolea waweze kusaidiwa kupata mbolea kwa urahisi kwa misimu mitatu mfululizo na badae wakajitegemee na kua mabalozi wazuri kwa wengine.

Mheshimiwa Mkuu wa mkoa amewataka TFRA kusogeza huduma za upatikanaji mbolea kwa kuweka matawi mkoani Lindi ili mbolea zipatikane kwa urahisi kupitia halmashauri za mkoa wa Lindi kama ilivo mikoa mingine kuliko ilivo sasa wakulima huagiza kutoka wilaya za Masasi  au Mtwara zinazopatikana mkoani Mtwara.

"Mnajua mkoa wa Lindi kuna maeneo  kubwa sana la uzalishaji lakin bado tija ya uzalishaji ni ndogo hivyo tuwaelimishe wakulima wetu kutumia maeneo au mashamba tuliyonayo kwa kutumia mbolea ili tupate mazao ya kutosha"amesema Bi Zainabu

Vilevile Mkuu wa Mkoa amekemea kitendo cha kilimo cha kuhamahama badala yake amewataka wataalam wa kilimo washirikiane vizuri na TFRA kuwaelimisha wakulima kuhusu kuzalisha mazao vizuri kwa kutumia mbolea katika eneo hilo hilo.

"Wanahamahama kwasababa wanafanya kilimo cha kizamani cha bila kutumia mbolea mkiwasiadia wakulima wetu kuwapa elimu zaidi ya matumizi ya mbolea kilimo cha kuhamhama kitaisha Mkoa wa Lindi

Aliendelea kuwasisitiza maafisa ugani kutumia vifaa watakavyopewa katika kuwasidia wakulima  kuanzia kupanda had kuvuna kwani hilo ni moja ya jukumu lao.

"mtapokea pikipiki 40 na zingine zitatolewa na bodi ya korosho hivyo zikatumike ipasavyo katika kutoa huduma bora za ugani, hizo pikipiki ni za kazi na si za kufanyia mambo binafsi zitumike kwa lengo husika" amesema Bi Zainab.

Mheshimiwa Zainab amewataka wakulima kuacha kuuza maua ya ufuta kipindi hiki na kusubiri ufuta uwe tayari ili wauze wakati wa msimu kwa mfumo wa stakabadhi ghalani.

" Haiwezekani  mkulima atumie nguvu, akili, muda na fedha katika kuzalisha ufuta alafu auze maua sasa hivi kwa shilingi elfu moja alafu mnunuzi wa maua yeye akauze ufuta uliyotayari  kwa shilingi  2,500/= jambo ambalo halikubaliki" amesema Bi Zainab.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania aliwataka wanakikundi walichopata elimu hiyo basi waendele kuitumia na kuwasaidia wengine ili kilimo cha mbolea kitumike kwa wingi  na wakazi wa Ruangwa.

"Sisi tunajivunia sana kuwasaidia wakulima wa Ruangwa na hatutoishia njiani tutaendelea kuwasaidia mpaka tuhakikishe matumizi ya mbolea Ruangwa yamefanikiwa kwa asilimia zote" amesema Dkt Stephan Ngailo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa