• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Awataka Wananchi Kumuunga Mkono Waziri Mkuu Katika Kushiriki Shughuli za Maendeleo.

Posted on: May 18th, 2017

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ,Mhe, Rashidi Nakumbya amewata wakazi wa Wilaya ya Ruangwa kumuunga mkono Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Kassim Majaliwa.

Amewataka wananchi kufanya kazi bega kwa bega na Mhe, Waziri katika kuleta maendeleo katika wilaya ya Ruangwa kwa Kushiriki shughuli za kimaendeleo alisema,maendeleo katika wilaya hii ni jukumu la kila mkazi wa eneo hili.

Alisema haya wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani lililofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia Mei 17 mpaka 18 katika ukumbi wa Rutesco mjini Ruangwa.


Mhe, Nakumbya aliwataka waheshimiwa Madiwani wa Wilaya ya Ruangwa kuhakikisha wanatumia nafasi zao katika kuhamasisha wananchi wao katika kuchangia kufanya shughuli za kimaendeleo katika kata zao.


“Nisiwe mchoyo wa kushukuru kama watu wamefanya vizuri basi ni wajibu wangu kuwapa pongezi, nawapongeza wananchi wa kata ya Nachingwea na Ruangwa kwa kazi nzuri ya waliyoifanya ya kujitolea katika ujenzi wa shule ya mpya ya Sekondari Kassim Majaliwa” alisema Mhe, Nakumbya.

Aidha alimtaka Mkurugenzi Mtendaji Andrea Chezue kuongea vizuri na  wachimbaji wa visima waliopo katika wilaya kwa ajili ya kuchimba visima, waanze na shule ya sekondari mpya kwani ikianza bila maji itakuwa shida kwa wanafunzi na walimu.

“Shule yetu ni nzuri sana ila itaendelea kuwa nzuri pale maji yatakapopatikana, maji ni uhai hatuwezi kuanza kutumia shule hiyo bila kuwa na maji kwani  itakuwa mateso kwa watoto wetu wakike pamoja na walimu ” alisema Mhe, Nakumbya.

Pia Mhe, Nakumbya aliwataka wananchi wa wilaya ya Ruangwa kuhakikisha wanasafisha mashamba yao ya mikorosho ili mgao wa dawa ya kupulizia utakapofika  kila Mkulima aweze kupata dawa hiyo na pia alisisitiza itazingatiwa zaidi kwa wale ambao wenye mashamba masafi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji Mhe, Eliasi Nkane aliwaomba wakuu wa shule na Afisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha wanafuatilia sheria ya mtoto anayeaacha kwani watoto hawa wasipochukuliwa hatua inasababisha kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wanaoacha shule.

“Zama za sasa imepunguza sana idadi ya watoto wa mitaani hivyo walimu na maafisa elimu ni wajibu wao kuwachukulia hatua watoto hawa wanaocha masomo ili tuzidi kutokomeza suala la watoto wa mtaani” alisema mhe Nkane.









Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa