• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MMAKIRU waaswa kuwa waadilifu

Posted on: December 21st, 2018

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Ruangwa  Rashidi Namkulala amewataka mtandao usio wa mashirika ya kiserikali (MMAKIRU) kuwa waadilifu wa mradi wa kuwawezesha vijana kutekeleza Sera za umma ya Sera ya maendeleo ya vijana kwa njia ya majukwaa ya vijana.

Ametoa rai hiyo kwenye utambulisho wa mradi huo uliofanyika leo desemba 21 mjini Ruangwa katika ukumbi wa CCM uliohudhuliwa na watendaji wa vijiji na kata tatu, madiwani na watendaji wa halmashauri.

Namkulala amesema mradi  huo umefadhiliwa na Foundation for Civil Society( FCS) ni wa shilingi milioni 49.5 ukiwa na lengo la kuwawezesha vijana kutekeleza Sera ya umma kupitia majukwaa ya vijana.

Afisa huyo aliwataka viongozi wa kata na Kijiji walioshiriki katika utambulisho huo wa mradi wakawe mabalozi wazuri katika kutoa elimu na lengo la mradi huo kwa vijana.

"Vijana wetu wanachangamoto nyingi mnatakiwa mjipange kukabiliana nazo ili mradi huu usije ukawa mradi hewa kama miradi mingine inayokwamishwa na vijana wenyewe " amesema Namkulala

Wakati huo huo Mwenyekiti wa bodi ya MMAKIRU aliiomba idara ya maendeleo ya jamii kuendelea mradi huo itakapofika mwisho wa wafadhiri kuwafadhili.

Alisema imekuwa  ni desturi ya miradi kutelekezwa na serikali inapoisha hivyo anaiomba serikali kuuendeleza mradi huo pale utakapokuwa umefika mwisho wa kufadhiliwa.

Pia aliwaomba vijana kupokea mradi huo na kuutumia kwa kadri ya maelekezo watakayokuwa wanapokea na mabalozi wao, pia  alichukua fursa hii kushukuru wafadhili wa mradi na kuwaomba waendele kuwasaidia pale wanapolekea miradi mingine.

Mradi huo ni wa shilingi milioni 49 na laki 5 umetolewa na wafadhiri na utawahusu vijana wenyewe rika la miaka 15 mpaka 35 na kwa kuanzia utaanza na kata 3 ambayo ni Nandagala,  Nkowe na Mandarawe.

MWISHO 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa