• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mhe, Majaliwa Akagua Ukarabati Shule ya Msingi Mnacho

Posted on: May 17th, 2017

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amekagua ukarabati wa majengo unaoendelea kufanyika katika shule ya Msingi Mnacho iliyopo Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

Shule hii ilianzishwa mwaka 1965 na kabla ya ukarabati kufanyika majengo yake yalikuwa hayapo katika hali nzuri. Mhe. Majaliwa akiwa ni mmoja ya wanafunzi ambao wamesoma hapo mwaka kuanzia mwaka 1970 alipoanza darasa la kwanza hadi la saba. Kutokana na uchakavu wa majengo hayo, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliamua kutafuta wafadhili ambao ndiyo wamesaidia kufanya ukarabati na sasa majengo ya shule yamebadilika.

Baada ya ukaguzi, Mhe. Majaliwa aliongea na viongozi, walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mnacho ambapo alianza kwa kuwapongeza walimu kwa uvumilivu waliouonesha kwa kufanya kazi katika mazingira ya majengo chakavu. Pia aliwapongeza kwa kazi nzuri ya ufundishaji wanayoendelea kuifanya.



Aidha, aliwaeleza kuwa pindi ukarabati huu utakapokamilika shule itakuwa imeimarika na kuwa na mwonekano mzuri. “Najua bado zipo changamoto kwenye upande wa nyumba za walimu ambazo nazo zinahitaji ukarabati, ila niahidi kwamba ukarabati huu ukishakamilika eneo litakalofuata ni ukarabati wa nyumba za walimu kuanzia nyumba namba moja hadi namba tano” alisema Mhe. Majaliwa.

Vilevile aliwasihi wanafunzi kusoma kwa bidi ili wakiwa wakubwa waweze kuja kushika nyadhifa mbalimbali kama yeye au hata zaidi. Pia aliwataka wanafunzi kuwaheshimu walimu wao na kuwa na nidhamu ya hali ya juu.



Kwa upande wa wananchi na viongozi waliokuwepo, Mhe. Majaliwa aliwaeleza kuwa ukarabati huu ni mwanzo wa ndoto aliyonayo ya kuboresha miundombinu ya shule hiyo. Aidha, amewasihi sana viongozi, wananchi na walimu kuwa na ushirikiano ili waweze kufanikiwa kuboresha elimu katika Wilaya nzima ya Ruangwa.

Pia Mhe. Majaliwa amewaomba waendelee kumuombea ili aweze kutimiza ndoto zake alizonazo za kuwa na Ruangwa yenye maendeleo na kuwa hilo litawezekana kama wana Ruangwa wote wataungana na kuwa kitu kimoja.




Ukaguzi huu wa shule aliufanya baada ya kumaliza kushiriki mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Kata ya Mnacho, Ndg Daniel Petro Mtawa ambae alifariki kutokana na ugonjwa wa moyo uliopelekea mwili kupooza upande mmoja.

Akiwa msibani aliwaomba watu kuendelea kumuombea marehemu, huku akiwasihi watu wote kujiandaa kama maneno ya mtumishi aliyoyasema ya watu kutenda matendo yaliyo mema yanayompendeza Mungu wakati wapo hapa duniani. “Nawapa pole sana wanafamilia, ndugu, jamaa, marafiki na madiwani kwa msiba huu uliotufika, msiba huu umetugusa sote kwani marehemu ni mtu ambaye tulikuwa tukishirikiana nae katika mambo mengi ya kimaendeleo katika wilaya yetu” alisema Mhe. Majaliwa.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa