• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAJALIWA AHIMIZA MSHIKAMANO KUIJENGA CCM

Posted on: October 2nd, 2022

MJUMBE wa Kamati Kuu na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Wana-Ruangwa waendelee kushikamana ili kukijenga Chama cha Mapinduzi (CCM) na kukifanya kibaki kuwa na nguvu.

 

“Nasisitiza haya kwa sababu hata Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wa Taifa, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametaka wanachama tushikamane tujenge upendo miongoni mwetu na tusimamie chama chetu ili kiwe na nguvu katika maeneo yetu,” amesema.

 

Mheshimiwa Majaliwa ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa ametoa wito huo leo (Jumapili, Oktoba 2, 2022) wakati akizungumza na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wilayani Ruangwa kutoka kata 22 uliofanyika ili kuwachagua viongozi wa wilaya hiyo.

 

“Kama eneo la Ruangwa litakuwa na nguvu, Nachingwea litakuwa na nguvu, Liwale litakuwa na nguvu, Kilwa litakuwa na nguvu, Lindi Vijijini na Manispaa yatakuwa na nguvu, mkoa wa Lindi automatically utakuwa na nguvu kisiasa na mimi naamini Ruangwa hatutamwangusha Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.”

 

Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwaeleza wajumbe wa mkutano huo mafanikio yaliyopatikana wilayani humo chini ya Serikali ya Awamu ya Sita ikiwemo ujenzi wa shule za msingi na sekondari, vituo vya afya, miradi ya maji, chuo cha VETA, mabweni ya wanafunzi wa sekondari, maji na umeme.

 

“Sisi wilaya ya Ruangwa tumetekeleza vizuri Ilani ya CCM na Rais Samia ametuunga mkono sana. Nani hajui kama wilaya hii ilikuwa na upungufu mkubwa kwenye sekta ya elimu? Nani hajui kwamba hatukuwa na shule za msingi katika kila kijiji? Lakini leo tumejitahidi na tumefikia zaidi ya asilimia 90. Ahadi ni kuhakikisha mpaka kufikia mwaka 2025, kila kijiji kinakuwa na shule ya msingi,” amesisitiza.

 

Akifafanua zaidi kuhusu elimu, Mheshimiwa Majaliwa amesema kulikuwa na kata tatu za Mbwemkuru, Nandagala na Nanganga ambazo zilikuwa hazina shule za sekondari lakini hivi sasa kila kata imepewa sh. milioni 470 na ujenzi umeshaanza.

 

“Pia tumepewa shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa shule maalumu ya wasichana watakaochukua masomo ya sayansi. Shule hii iko Ruangwa, nyuma ya uwanja wa mpira wa Majaliwa na itaanza kufundisha kuanzia Januari, 2023.”

 

Amezitaja shule nyingine zilizojengwa kuwa ni ya Kitandi ambayo pia itaanza kufundisha kuanzia Januari, 2023. “Wilaya hii, watoto wetu wa kike bado wana changamoto nyingi, kwa vile Liugulu kuna sekondari mbili, tumeamua moja iwe na wavulana na nyingine iwe ya wasichana na zote hizi tunazijengea mabweni ili vijana wetu wapate malezi mazuri shuleni.”

 

Amesema wilaya hiyo ilipokea sh. bilioni mbili za ujenzi wa Chuo cha VETA na kuwaarifu wajumbe hao kwamba wamepata eneo la ekari 70 na ujenzi wake umekamilika isipokuwa wanasubiri kuingiza maji.

 

Kuhusu afya, Mheshimiwa Majaliwa amewaeleza wajumbe hao kuwa ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo imefikia hatua nzuri na vituo vya afya vya Luchelegwa, Nandagala, Ruangwa, Narung’ombe, Nangurugai, Namichiga na Mandawa umekamilika. “Itabakia kata moja ya Nambilanje,” amesema.

 

Kuhusu umeme, Mheshimiwa Majaliwa amesema kazi ya kusambaza umeme vijijini inaendelea na lengo la wilaya ni kuhakikisha ifikapo Desemba 2022, vijiji vyote viwe vimepata umeme.

 

Uchaguzi bado unaendelea wa kuwachagua Mweyekiti wa CCM wa Wilaya, Wajumbe watatu wa Mkutano Mkuu Taifa, Wajumbe 10 wa Halmashauri Kuu ya Wilaya na Wajumbe wawili wa Halmashauri Kuu ya Mkoa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa