• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

LIDEO YAWAJENGEA UWEZO MAKUNDI MAALUMU KATIKA MAWASILIANO NA MAENDELEO

Posted on: September 13th, 2024
  1. Asasi isiyo ya kiserikali ya Lindi Deaf Organization (LIDEO) imetoa semina maalumu kwa ajili ya makundi yenye mahitaji maalumu, lengo likiwa ni kuwaelimisha kuhusu mawasiliano ya lugha ya alama pamoja na kushiriki katika shughuli za maendeleo kijamii, kiuchumi, na kiutamaduni, semina hiyo imefanyika leo, Septemba 13, 2024, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.


Mgeni rasmi kwenye semina hiyo amekuwa Mheshimiwa Msoga Matiku Magari, aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mheshimiwa Hassan Ngoma, semina imehudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo watu wenye mahitaji maalumu, Maafisa wa Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, pamoja na wawakilishi kutoka idara ya mahakama na jeshi la magereza.


Akizungumza kwenye semina hiyo, Ndugu Matiku amesema kuwa Serikali inatambua umuhimu wa makundi maalumu na imeweka mikakati ya kuwasaidia kujikwamua kiuchumi na kijamii. Aidha, amewatia moyo wanajamii hao kuchangamkia fursa za kugombea nafasi za uongozi kwenye Serikali za Mitaa katika uchaguzi wa mwaka huu. 

"Wazazi wanapaswa kuwatoa hadharani watoto wenye mahitaji maalumu, kwani Serikali inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa shule maalumu na kuboresha huduma kwa kundi hili," amesema Matiku.


Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa LIDEO, Ndugu Jaafari Murtaza, ameongeza maelezo kuhusu malengo ya asasi hiyo, akibainisha jitihada zao za kuendeleza kituo cha mafunzo ya lugha ya alama kilichopo Ngongo, Lindi. Ameongeza kuwa LIDEO inajihusisha na kutoa fursa za mafunzo na miradi ya kijamii kama vile kilimo na umiliki wa ardhi kwa makundi maalumu.


Naye, Afisa manunuzi kanda ya kusini amesema  kuzingatia umuhimu wa makundi maalumu Serikali imezitaka taasisi nunuzi kutenga asilimia 30 % ya bajeti ya ununuzi wa umma kwa makundi maalumu ili kukuza ajira binafsi na ujasiriamali .


Kupitia risala iliyosomwa na Alice Namwembe, LIDEO imeainisha changamoto zinazoikabili asasi hiyo, zikiwemo ukosefu wa wadau wa kuwaunga mkono katika kukamilisha ujenzi wa darasa kwa watu wenye mahitaji maalumu katika Manispaa ya Lindi. Namwembe amependekeza Serikali itenge maeneo maalumu kwa gharama nafuu ili kusaidia makundi hayo kumiliki ardhi na kukuza ustawi wao


Kwa ujumla, semina kama hizi ni muhimu katika kuimarisha ushirikishwaji wa makundi maalumu kwenye shughuli za maendeleo, hatua iliyokuwa ikikosekana kwa muda mrefu. Hivi sasa, jitihada za Serikali na asasi kama LIDEO zinaonekana kuwa na matokeo chanya, lakini changamoto za miundombinu na upungufu wa wadau bado zinahitaji kushughulikiwa. Ikiwa mipango madhubuti itawekwa, mustakabali wa makundi maalumu unaweza kuwa wenye matumaini zaidi, kwa kuhakikisha wanapata nafasi sawa za kushiriki katika kila nyanja ya maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • TAARIFA KWA UMMA

    June 04, 2025
  • WANAFUNZI RUANGWA WAIBUKA KIDEDEA USAFI NA UNADHIFU UMISSETA 2025 MKOA WA LINDI

    June 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA NISHATI SAFI WANDORWA

    May 28, 2025
  • RUANGWA YAPOKEA MWENGE WA UHURU 2025 KUTOKA LINDI MANISPAA

    May 28, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa