• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Dc Mgandilwa amewataka wananchi Ruangwa kujitoa katika shughuli za maendeleo

Posted on: December 4th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa  Mhe. Hashim Mgandilwa amewataka wananchi wote wa Wilaya ya Ruangwa kujitoa hali na Mali katika kuchangia shughuli za maendeleo zinazoendelea katika maeneo yao.


Ameyasema hayo alipokuwa kwenye muendelezo wa ziara zake  katika kata ya Nandagala siku ya tarehe 04/ 12/2018 alipokuwa akiongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara


Mhe. Mgandilwa amewataka wananchi kuanza kutatua changamoto zilizopo katika maeneo yao ambazo aziitaji fedha mfano barabara ambayo inahitaji nguvu kazi kwa kukata visiki na kutoa manyasi.


" Tusisubiri kuletewa maendeleo tuanze wenyewe kuyaleta najua maeneo mengi mnaupungufu wa  vyumba vya madarasa anzeni kufyatua matofali na ujenzi wa awali, Serikali itatia nguvu kazi kama sehemu nyingine"


"Mtakapopanga siku  yakufanya hizo kazi nipeni taarifa nitakuja kufanya kazi na nyie na mie ni kiongozi nisiyependa kukaa ofisini nitakuja na watu wangu kwani sisi viongozi ndiyo tunapaswa kuwa mfano" alisema


Kuhusiana na Ujenzi wa shule ya Sekondari ya Mnacho Mhe. Mgandilwa amewataka wakazi wa kata ya Nandagala kuchangia ujenzi wa mabweni ya shule ya Sekondari Mnacho


Kwani kukamilika kwa Ujenzi huo kutapunguza adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kutafuta elimu


"Ujenzi wa mabweni katika shule ya Mnacho ni jukumu la kila mkazi wa kata ya Nandagala na Mnacho najua vipo vitu mmekubalina kufanya vya kimaendeleo vya kata zenu na ni vya umuhimu ila ujenzi wa mabweni ni muhimu zaidi" amesema Mgandilwa


Vilevile Mkuu wa Wilaya ametoa onyo  kwa wanawake wote ambao wanacheza michezo ya kukaa uchi katika sherehe mbalimbali zinazofanyika katika Wilaya ya Ruangwa


Nipeni taarifa ya mtu yoyote anaefanya hiyo michezo ya kukaa na kucheza michezo  isiyokuwa na maadili nitakushughulikia nikikubaini.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa