• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA ROBO YA PILI 2025/2026

Posted on: January 29th, 2026


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa limekaa leo, tarehe 29 Januari 2026, katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri, kujadili na kupitia taarifa za utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni sehemu ya wajibu wake wa kisheria wa kusimamia rasilimali za umma na utekelezaji wa miradi.


Katika kikao hicho, taarifa za kamati zote za Halmashauri ziliwasilishwa na kujadiliwa, huku Madiwani wakitoa maoni, kuuliza maswali na kupendekeza maboresho kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kata zote 22 za Wilaya hiyo.


Awali, akifungua Baraza hilo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Fadhily Bakari Mbwelei, ameeleza mwelekeo wa uongozi wake kwa kipindi cha miaka mitano, akisisitiza mshikamano kati ya Madiwani na wataalamu wa Halmashauri ili kufanikisha maendeleo kwa wananchi.


Amesema uongozi wake utahakikisha miradi viporo na inayoendelea inatembelewa na kukaguliwa mara kwa mara hadi ikamilike, huku masuala ya michezo, ziara za mafunzo, utekelezaji wa sera na ilani, pamoja na ulinzi na usalama yakipewa kipaumbele. Aidha, amewahimiza viongozi kuepuka utendaji wa mazoea na kuweka mbele maslahi ya wananchi.


Akizungumza katika Baraza hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndg. Ernest Haule, amesema uongozi utaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa mipango ya maendeleo kwa kushirikiana na Madiwani na wadau wengine ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati.


Naye Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Ndg. Juma Mpanda, amewasilisha salamu za Mbunge, akieleza kuwa anaunga mkono juhudi za Halmashauri katika kusukuma ajenda za maendeleo na kuhimiza ushirikiano kati ya viongozi wa kuchaguliwa na wataalamu wa Serikali.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • RUANGWA YASHIKA NAFASI YA KWANZA MKOA WA LINDI MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2025

    January 18, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA ROBO YA PILI 2025/2026

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA MAENDELEO YA KATA

    January 28, 2026
  • WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA e-UTENDAJI (WATUMISHI)

    January 29, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa