• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA MAENDELEO YA KATA

Posted on: January 28th, 2026




Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa limekaa leo, tarehe 28 Januari 2026, katika Ukumbi Mkubwa wa Mikutano wa Halmashauri, ambapo Madiwani wa Kata zote 22 wamejadili na kuwasilisha taarifa za maendeleo ya kata zao, zikibainisha mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa miradi.


Mkutano huo wa Baraza umehudhuriwa na wataalamu kutoka Idara/Vitengo mbalimbali vya Halmashauri pamoja na taasisi za umma ambapo wamepata fursa ya kujibu hoja, maswali, na kutoa maelekezo yanayohusu utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika Kata mbalimbali.


Akijibu hoja za Waheshimiwa Madiwani kuhusu utekelezaji wa miradi na shughuli za maendeleo ngazi ya kata, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndg. Ernest Haule, aliweka bayana hatua zinazochukuliwa na Halmashauri ili kuhakikisha malengo ya maendeleo yanatekelezwa kwa ufanisi.


“Tunaendelea kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa malengo ya maendeleo kwa maslahi ya wananchi wetu wote.” Amesema Haule.


Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mhe. Fadhily Bakari Mbwelei, amesema kuwa uwasilishaji wa taarifa za Kata ni nyenzo muhimu ya kupima maendeleo halisi yanayogusa wananchi moja kwa moja. Amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Madiwani, wataalamu, na wananchi katika kutatua changamoto zilizopo, na kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia thamani ya fedha.


Aidha, katika mkutano huo Waheshimiwa Madiwani wamesisitiza utekelezaji wa miradi ya maji safi na salama, ujenzi na matengenezo ya barabara, pamoja na kuendelea kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, hatua inayolenga kuimarisha uwajibikaji na usimamizi wa maendeleo ngazi ya kata.


Mkutano huo ni kielelezo cha jitihada za Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa za kuimarisha uwazi, uwajibikaji, na ushirikiano kati ya madiwani, wataalamu, na wananchi, kwa lengo la kuhakikisha miradi ya maendeleo inakidhi mahitaji halisi ya jamii na kutoa matokeo chanya kwa maendeleo endelevu ya kata zote wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • RUANGWA YASHIKA NAFASI YA KWANZA MKOA WA LINDI MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2025

    January 18, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA ROBO YA PILI 2025/2026

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA MAENDELEO YA KATA

    January 28, 2026
  • WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA e-UTENDAJI (WATUMISHI)

    January 29, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa