• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKUU WA WILAYA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYABIASHARA RUANGWA

Posted on: November 18th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mheshimiwa Hassan Ngoma, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyabiashara Wilaya ya Ruangwa, ameongoza kikao cha baraza hilo leo, tarehe 18 Novemba 2024, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya.


Kikao hicho kimehusisha viongozi wa wafanyabiashara na wadau wengine muhimu kutoka makundi mbalimbali, wakijadili masuala ya biashara na maendeleo katika Wilaya ya Ruangwa, hata hivyo Kikao cha Baraza la Wafanyabiashara Wilaya ya Ruangwa kimekuwa jukwaa muhimu la kujadili changamoto zinazowakabili wafanyabiashara, kubuni mbinu za kuboresha mazingira ya biashara, na kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Wilaya hiyo.


Aidha, Wakati wa kikao hicho, Mh. Ngoma ametumia fursa hiyo kuhimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024.


Katika hotuba yake, Mh. Ngoma amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, huru, na utulivu, akitoa wito kwa wananchi kutanguliza mshikamano na heshima wakati wa mchakato wa uchaguzi.


“Kupiga kura ni kitendo cha siku moja. Itakapofika saa 12:00 jioni ya tarehe 27 Novemba mwaka huu, kila kitu kitakuwa bayana mshindi atajulikana na atakayeshindwa atajulikana. Kwa hiyo, chochote utakachokifanya, kiwe cha kheri na si kuacha makovu kwenye mioyo ya watu,” amesema.


Mbali na hayo, Mhe. Ngoma amewakumbusha wananchi kwamba uchaguzi ni tukio la muda mfupi, lakini maisha ya kijamii yataendelea baada ya uchaguzi, hivyo kuwataka kuzingatia ustawi wa jamii na kuepuka vitendo vya uvunjifu wa amani.


“Uchaguzi utaisha, lakini sisi tunaendelea kuishi pamoja. Endapo utasababisha madhara kwa mtu au familia, utamtazamaje baada ya uchaguzi?” ameongeza Mh. Ngoma kwa kusisitiza mshikamano wa kijamii.


Kikao cha Baraza la Wafanyabiashara kimehitimishwa kwa maazimio yanayolenga kuboresha mazingira ya biashara na kukuza uchumi wa Wilaya ya Ruangwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa