Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imegawa komputa mpakato (laptop) kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wote ili kuimarisha matumizi ya TEHAMA na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi, katika hafla iliyofanyika leo Februari 18, 2026 kwenye bwalo la Shule ya Sekondari ya Wasichana Ruangwa, .
Vifaa hivyo vimekabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, kwa kushirikiana na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Ndg. Rashid Namkulala.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, mhe. Ngoma amesema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za serikali kuimarisha utendaji kazi kwa njia za kidigitali, akieleza kuwa komputa hizo zitasaidia kuongeza kasi ya ukusanyaji wa takwimu, ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa taarifa kwa wakati.
Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Ndg. Namkulala amewataka maafisa waliopokea komputa mpakato kuzitumia kwa uadilifu na weledi, kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, ili ziwe na matokeo chanya kwa jamii.
Baadhi ya Maafisa Maendeleo ya Jamii walioshiriki hafla hiyo wametoa shukrani kwa uongozi wa Wilaya na kuahidi kutumia vifaa hivyo ipasavyo kuboresha utekelezaji wa majukumu yao katika ngazi ya kata.
Ugawaji wa komputa mpakato ni sehemu ya mkakati wa kuharakisha mabadiliko ya kidigitali katika utoaji wa huduma na usimamizi wa shughuli za maendeleo wilayani humo.
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa