• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DC NGOMA: WANAFUNZI WOTE WASIORIPOTI SHULE MWISHO WA KURIPOTI NI JUMATATU

Posted on: January 30th, 2026




Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, amewaagiza wazazi na walezi kuhakikisha wanafunzi wote ambao bado hawajaripoti shuleni wanarejea mara moja kabla ya siku ya Jumatatu, akionya kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaokaidi agizo hilo.


Agizo hilo lime­tolewa leo, tarehe 30 Januari 2026, wakati wa kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kikiwahusisha Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Elimu wa Kata, Watendaji wa Kata na Vijiji na Kamati ya Ulinzi na usalama Wialaya, kwa lengo la kufanya tathmini ya mwenendo wa kuripoti shuleni na mahudhurio ya wanafunzi wa awali, msingi na sekondari.


Katika kikao hicho, Maafisa Elimu wamewasilisha taarifa kutoka kata zote 22, zikionesha idadi ya wanafunzi ambao bado hawajaripoti shuleni licha ya mwaka wa masomo kuanza.


Akizungumza baada ya kusikiliza taarifa hizo, Mhe. Ngoma amesema Serikali haitavumilia uzembe au kisingizio chochote kinachozuia watoto kupata haki yao ya msingi ya elimu. Amesisitiza kuwa elimu ni bure, hivyo hakuna sababu ya kuwazuia watoto kwenda shule.


“Nawagiza nyote kuhakikisha watoto ambao hawajaripoti shuleni wote wanaripoti. Hakikisheni wazazi wanawapeleka wote maana elimu ni bure. Asiwepo mtu wa kuleta kisingizio chochote. Siku ya Jumatatu ndiyo mwisho, wanafunzi wote waripoti shule walizopangiwa na kuandikishwa,” amesema Mhe. Ngoma.


Aidha, Mkuu wa Wilaya amesisitiza uadilifu kazini, kufanya kazi kwa bidii, kulinda taswira ya Serikali, kuepuka vitendo vya rushwa na propaganda zisizo za kweli, pamoja na kutenda haki kwa wananchi.


“Twendeni 2026 tukaichore taswira sahihi ya Serikali yetu, tukatoe huduma bora za kiuongozi kwa wananchi wetu. Kila mtu afanye kazi yake kwa usahihi ili tuone matokeo ya kazi zetu,” amesema.


Kikao hicho kimebainisha dhamira ya Serikali ya Wilaya ya Ruangwa kuhakikisha kila mtoto anapata elimu kwa wakati na kwamba ushirikiano wa wadau wote unahitajika ili kufanikisha azma hiyo.

Matangazo

  • FOMU YA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI February 02, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA WILAYA YA RUANGWA YAFANYIKA LEO

    February 02, 2026
  • RUANGWA YASHIKA NAFASI YA KWANZA MKOA WA LINDI MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2025

    January 18, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA ROBO YA PILI 2025/2026

    January 29, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI RUANGWA LAJADILI TAARIFA ZA MAENDELEO YA KATA

    January 28, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa