• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

ZIMA MOTO WAENDESHA MAFUNZO YA TAHADHARI YA MAJANGA KWA WATUMISHI RUANGWA

Posted on: July 15th, 2025

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Ruangwa limeendesha mafunzo ya kinga na tahadhari kwa watumishi wote wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, leo tarehe 15 Julai 2025. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo kwa lengo la kuwajengea uelewa wa awali kuhusu namna ya kukabiliana na majanga kazini na majumbani.


Wakiendesha mafunzo hayo, SGT Richard Fredrick Urembo pamoja na FC Petro Simon Makalwe wamesema elimu hiyo imekusudiwa kuwapa watumishi maarifa ya kuzuia majanga kama moto, gesi na ajali za papo kwa papo. Aidha, wamefafanua kuwa hatua za haraka za awali huokoa maisha na mali kabla ya msaada wa kitaalamu kufika.

Kwa mujibu wa wawezeshaji hao, uelewa wa kinga dhidi ya majanga umebainika kuwa moja ya nguzo muhimu ya usalama kazini, wameeleza kuwa mara nyingi madhara makubwa hutokea kutokana na ukosefu wa maandalizi, vifaa sahihi au ujuzi wa kutumia njia salama wakati wa dharura.


Sambamba na hayo, watumishi wamefundishwa kwa usahihi namna ya kutumia kizimia moto, kufahamu aina mbalimbali za moto na namna ya kuuzima kulingana na chanzo chake. Pia, wameelekezwa hatua za msingi za kutoa msaada wa haraka kwa mtu aliyejeruhiwa katika tukio la moto au tukio la dharura.


Akizungumza kwa niaba ya Halmashauri, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mhe. Adv. Zuberi Sarahani amepongeza Jeshi la Zimamoto kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo amesema yamewafumbua macho watumishi wengi kuhusu hatari walizokuwa hawazifikirii kila siku.


“Mafunzo haya yamekuwa msaada mkubwa, yameongeza uelewa wa tahadhari kwa mazingira yetu ya kazi na hata majumbani, ni matumaini yangu kuwa yataendelea kufanyika mara kwa mara kwa kuwa usalama ni jambo la msingi kwa maendeleo ya taasisi,” amesema Adv. Zuberi.

Mafunzo hayo yamehitimishwa kwa mazoezi ya vitendo ambapo watumishi wamejifunza namna ya kutumia kizimia moto (fire extinguisher), mbinu za kujiokoa na kuwasaidia wengine, ikiwa ni hatua ya kuimarisha usalama na utayari wao wa kukabiliana na majanga yanapojitokeza kwa ghafla katika mazingira ya kazi na nyumbani.


Kwa ujumla, mafunzo hayo yameongeza ari na uelewa miongoni mwa watumishi kuhusu wajibu wao katika kuhakikisha mazingira yao yanakuwa salama dhidi ya majanga. Halmashauri imedhamiria kuendelea kushirikiana na taasisi za uokoaji katika kujenga utamaduni wa tahadhari na uwajibikaji.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • ZIMA MOTO WAENDESHA MAFUNZO YA TAHADHARI YA MAJANGA KWA WATUMISHI RUANGWA

    July 15, 2025
  • MAAFISA MIFUGO RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO KUELEKEA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO

    July 11, 2025
  • MAAFISA MIFUGO RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO KUELEKEA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO

    July 11, 2025
  • PONGEZI

    July 11, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa