
Timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, ASHALONGO FC, na KIBWANA FARM FC kutoka Mibure, zimetoshana nguvu kwa sare ya mabao 2–2 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo, tarehe 08 Februari 2026, saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Majaliwa.
Katika mchezo huo wenye ushindani mkubwa, ASHALONGO FC walitangulia kupata bao la kwanza, kabla ya KIBWANA FARM FC kusawazisha na kuufanya mchezo uwe wa kasi na mvuto mkubwa.
KIBWANA FARM FC waliongeza bao la pili na kuonekana kuelekea ushindi, lakini ASHALONGO FC waliinuka na kusawazisha kupitia shambulizi la haraka lililowainua mashabiki wao.
Licha ya mashambulizi ya pande zote katika dakika za mwisho, hakuna timu iliyofanikiwa kuongeza bao, na filimbi ya mwisho ikapulizwa huku matokeo yakibaki sare ya 2–2. Hata hivyo KIBWANA FARM FC wameahidi kujipanga upya na kurejea kwa awamu nyingine ili wapate ushindi.
Mchezo huo wa kirafiki ulilenga kuimarisha uhusiano kati ya timu hizo, kukuza vipaji vya wachezaji na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa michezo katika kuimarisha afya na mshikamano.
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa