• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WILAYA YA RUANGWA YAANDAA BONANZA KUELEKEA MIAKA 63 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Posted on: December 7th, 2024

Wilaya ya Ruangwa imefanya bonanza la michezo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kilele cha maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara, ambayo Wilayani Ruangwa yatafanyika kesho tarehe 8 Desemba, bonanza hilo limefanyika leo tarehe 7 Desemba 2024, likihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, rede, bao, na kuvuta kamba, kwa lengo la kuimarisha mshikamano wa kijamii na kusherehekea mafanikio ya Taifa.


Aidha, mashindano ya mpira wa miguu yamezua msisimko mkubwa, ambapo mchezo wa kwanza umezikutanisha timu za Kiwengwa na Ruangwa Boys, timu ya Kiwengwa imeibuka mshindi kwa mabao 3-1. Katika mchezo wa pili, Bodaboda kwa Wanyumbani imepoteza kwa mabao 5-2 dhidi ya Pachenga, hivyo basi timu za Kiwengwa na Pachenga zitakutana katika fainali, itakayofanyika kesho, tarehe 8 Desemba, katika viwanja vya Shule ya Msingi Likangara.


Hata hivyo, michezo mingine kama rede, bao, na kuvuta kamba nayo imefanyika kwa hamasa kubwa, washiriki na mashabiki wameshirikiana kuonyesha mshikamano, huku vikundi vya michezo vikifanya vizuri na kuvutia umati wa watazamaji.


Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Matiku Msonga, amesema kuwa bonanza hilo limeonesha ushirikiano wa hali ya juu miongoni mwa wananchi.


 “Tunaendelea kuhimiza michezo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuhamasisha uzalendo. Nawapongeza washiriki wote waliojitokeza kushiriki na kufanikisha tukio hili,” amesema Msonga.


Vile vile, maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu inayosema: “Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara – Uongozi Madhubuti na Ushirikishwaji wa Wananchi ni Msingi wa Maendeleo Yetu.”Kauli mbiu hii inahimiza mshikamano wa kitaifa na umuhimu wa kushirikiana katika maendeleo.


Ikumbukwe, Shughuli hizi zinaendelea kuleta hamasa kubwa kuelekea kilele cha sherehe za Uhuru, ambapo wakazi wa Wilaya ya Ruangwa wanatarajiwa kushiriki kwa wingi katika tukio hili la kihistoria.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa