• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Waziri Mkuu awataka askari kata wazingatie maadili

Posted on: November 22nd, 2021

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka  Askari Kata wafanye kazi kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya utumishi waona waache tabia za ubabe na vitisho kwani zitaleta mpasuko kati yao na wananchi na hatimaye watashindwa kutekeleza majukumu yao.

Pia, Waziri Mkuu amewataka Watendaji wote wa Kata, Vijiji, Mtaa na Vitongoji waimarishe mifumo ya udhibiti kwa kuanzisha na kutumia daftari lenye orodha ya wakazi. “Wekezi mifumo ya kujua nani ameingia na lini atatoka kwenye mitaa yenu ili kubaini viashiria vyote vya usalama.”

Ametoa msisitizo huo leo (Jumatatu, Novemba 22, 2021) wakati akifungua Mafunzo ya Watendaji wa Kata na Vijiji yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi Tanzania na Taasisi ya Hanns Seidel Foundation (HSF), Ruangwa mkoani Lindi.

Waziri Mkuu amesema askari hao wasipofanya kazi kwa kuzingatia maadili watashindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo, amewasisitiza waimarishe uhusiano mwema wa kikazi na wananchi wanaowatumikia na wasiwe chanzo cha uvunjifu wa amani.

Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi wawapokee Askari Kata katika maeneo yao na kwamba hao si adui zao bali ni marafiki ambao wanawahitaji katika kutenda kazi zao, hivyo wawape ushirikiano mkubwa katika masuala yote ya ulinzi na usalama.

Amesema Serikali imeridhia mafunzo hayo yafanyike kwa kujua umuhimu wake kwao, hivyo ni anatarajia watayapa umuhimu mkubwa kama inavyotakiwa. “Utaratibu uwekwe ili watendaji wa ngazi ya kata za vijiji katika kila halmashauri nchini wapate mafunzo haya.”

Waziri Mkuu amesema kuwa ana imani kupitia mafunzo hayo watendaji hao watapata ujuzi na maarifa ambayo yatawajengea fikra chanya kuhusu suala la ulinzi na usalama na hatimaye watakuwa wazuri zaidi

“Na matarajio ya Serikali ni kwamba mtaenda kufanyakazi kwa kuzingatia yote mtakayoyapata kutokana na mafunzo haya. Mafunzo haya yatawawezesha kutekeleza kikamilifu majukumu mahsusi ikiwemo kuwezesha na kudumisha utulivu, amani na utawala bora.”

Pia Waziri Mkuu amesema baada ya mafunzo hayo watendaji hao wanapaswa kuwa kiungo bora na Jeshi la Polisi ili waendelee kudumisha uhusiano mwema baina yao na wananchi wanaowatumikia.

“Uhusiano mwema utawafanya wananchi wawaamini na wawe huru kuwapa ushirikiano wote mnaohitaji katika kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yenu ya utendaji. Kaimarisheni uhusiano wa wananchi na Jeshi la Polisi ili tuweze kufanikiwa kuwa na jamii yenye imani na Jeshi letu, hivyo kuwa na utayari katika kushiri kulinda amani na usalama wa watu na mali zao”

Mheshimiwa Majaliwa  amesema kuwa wadau wote wa masuala ya ulinzi na usalama kwa pamoja washirikiane katika kujenga mazingira mazuri ya wananchi kushiriki katika kujilinda wenyewe pamoja na mali zao.

“Pamoja na hilo pia toeni ushirikiano mkubwa kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama na hatimaye kuendelea kudumisha azma ya Serikali yetu ya kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kisiwa cha amani”

Naye, Kamishina wa Ushirikishwaji wa Jamii kutoka Jeshi la Polisi, Dkt Mussa Ali Mussa amesema utekelezaji wa mradi huo wa Polisi Kata ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi yenye lengo la kuhakikisha wanaweka uhusiano wa karibu wa kiutendaji kati ya Polisi, Watendaji wa kata pamoja na Madiwani.



Awali, Mkurugenzi Mkazi wa taasisi ya Hanns Seidel Foundation Tanzania na Uganda Karl Peter Schoenfisch amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwafanya wananchi kutambua wajibu wao katika jamii zao na kuweza kutoa ushirikiano kwa Askari Kata kila inapohitaji, hivyo kupunguza uhalifu katika maeneo yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa