• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wanawake Msiwakatishe Watoto Masomo

Posted on: March 8th, 2018

Wanawake Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi wametakiwa kuacha tabia ya kuwakatisha watoto ndoto zao hasa wanafunzi wa shule za msingi kwa kuwataka wajifelishe katika mitihani ya darasa la saba, kwa kigezo cha kutokuwa na uwezo wa kuwasomesha kujiunga elimu ya sekondari.

Hayo yamesemwa na Afisa wa kuzuia na kupambana na Rushwa Bi, Angela Mwabulambo alipozungumza mbele ya kina mama katika viwaja wa CWT Ruangwa wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, ambayo uadhimishwa duniani kote kila ifikapo machi 8.

Amesema Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa imekuwa na utaratibu kuandaa club za kupambana na rushwa kwa wanafunzi za msingi na sekondari, lengo kubwa likiwa ni kuwajenga watoto katika misingi ya uzalendo wa kuepuka na kukemea masuala ya rushwa jinsi yanavyopoteza haki.

“Tunapowahoji watoto na kutaka kujua sababu za wao kufanya vibaya katika mitihani yao wanafunzi wengi wameeleza kuwa wameambiwa na wazazi wao hasa kina mama kuwa wajifelishe kwani wao hawana uwezo wa kuwasomesha elimu ya juu” amesema Bi. Angela

Kutokana na taarifa hizo Bi, Angela amesema kufanya hivyo ni kumnyima mtoto haki yake ya msingi ya kupata elimu na kuwaomba wadau washirikiane kutolea taarifa matukio hayo katika vyombo vya sheria huku akiwahimiza wamama wapende watoto wao kwa kwa kuwapa elimu, kwani elimu ndiyo urithi pekee wa kueleweka kwa mtoto.

Wakati huo huo mlezi wa dawati la jinsia kutoka kituo cha polisi cha Ruangwa Afande Mpokigwa Mwamulanga amewataka wamama kufichua matukio ya unyanyasaji wanaotendewa kwa kutoa taarifa katika kituo cha polisi ili kutokomeza hali ya unyanyasaji wa kijinsia kwa kwa wanawake.

Aidha amesema matendo mengi yanafanyika ya kikatili kwa wanawake lakini kina mama wengi wamekuwa wakiyanyamazia na wengine hata kutokujua huku akitaja mifano ya matendo hayo kuwa pamoja na kupigwa, kutukanwa, kukashifiwa na kushikwashikwa sehemu yoyote ya mwili bila ridhaa.

Baadhi ya wanawake waliohudhuria wameeleza kuhusu kuhamasika kwao kushiriki katika shughuli mbalimbali za ujasilimiamali kama utengenezaji wa sabuni, batiki, ushonaji na kuwahimiza wanawake wengine kutobweteka katika shughuli kwani maendeleo hutokana na bidii ya kazi.

Kauli mbiu ya mwaka huu nchini Tanzania inasema kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe usawa, jinsia na uwekezaji wanawake vijijini, kauli hii inakuja ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa