• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wakurugenzi lipeni stahiki za watumishi- RC Zambi

Posted on: May 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mheshimiwa Godfrey Zambi amewataka Wakurugenzi wakulipa mishahara ya watumishi kwa wakati wanaolipwa kwa fedha za mapato ya ndani.

Pia amewataka waajiri wa taasisi binafsi  kuzingatia haki za wafanyakazi wao kwa kulipa maslahi ya wafanyakazi hao kwa wakati.

Ameyasema hayo leo Mei 1/2019 wakati wa maadhimisho ya mei mosi yaliyofanyika katika viwanja wa shule ya mpilipili Mkoani lindi mjini.

"Stahiki zipo nyingi ni wajibu wenu waajiri kutoa stahiki hizo anzeni na kuwapa vitendea kazi ili waweze kutimiza wajibu wao kama inavyotakiwa" amesema mheshimiwa Zambi.

Vile vile amewataka watumishi kuwa na imani na serikali ya awamu ya tano kwani inashughulikia na inaendeleza kusimamia haki za watumishi na zoezi la upandaji wa madaraja unaendelea.

"Rais wetu John Pombe Magufuli ni mtetezi wa haki za wanyonge anahakikisha kila mtu anapata stahiki yake fanyeni kazi mkiwa na imani na Rais kwani hatoacha kuwatimizia mahitaji yenu" amesema Zambi

Aidha amewataka wafanyakazi wa serikali na wataasisi binafsi kupinga vitendo vya rushwa katika maeneo yao ya kazi na ikitokea hali ya rushwa katika maeneo yenu ya kazi mpeleke malalamiko hayo katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa katika maeneo yenu ya kazi.

"Serikali ya sasa haitaki mchezo ukibainika unaomba au kupokea rushwa sitokuvumilia hatua kali za kisheria zitafuata kwa kufuata taratibu mtumishi kaa mbali na rushwa ni adui wa maendeleo "amesema Zambi

Wakurugenzi simamieni hivi vigezo cha mfanyakazi hodari ili watu waache kupeana tu kuwa kufuata nani mwaka jana kapata mwaka mwingine apate mwingine hata kama mtu amepata mara tatu na anasifa basi apate huyo huyo na si kupeana bila kuangalia vigezo muhimu.

Naye Mratibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi TUCTA bi Fatma Chiwonga amewaomba waajiri kuwasaidia wafanyakazi waliostaafu wanapata stahiki zao kwa wakati.

Pia ameiomba serikali kupunguza makato ya kodi kwa watumishi kutoka asilimia 9 mpaka asilimia 6 kwani kiwango cha makato ya sasa ni kikubwa sana.

"wafanyazi wanafanya kazi katika mazingira magumu tuwafanyieni unafuu hata kidogo haya makato kutokana na mishahara wanayopokea makato hayo yamekuwa ni makubwa" amesema bi Fatma.

Maadhimisho hayo kimkoa yamefanyika manspaa ya Lindi iliyopo Lindi mjini, Maadhimisho hayo yamebeba ujumbe wa "Tanzania ya uchumi wa kati inawezekana wakati wa mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi ni sasa"

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa