• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WAJUMBE WA SERIKALI ZA VIJIJI KATA YA NANDAGALA WAJIPONGEZA KWA KAZI NZURI YA NDANI YA MIAKA MITANO YA UONGOZI WAO

Posted on: August 13th, 2024

Wajumbe wa Serikali za Vijiji vya Kata ya Nandagala wamefanya sherehe ya kujipongeza kwa utumishi wao uliotukuka kwa kipindi cha miaka mitano tangu waingie madarakani. Sherehe hiyo imefanyika Agosti 12, 2024, katika bwalo la Chuo cha VETA Nandagala, kilichopo Kata ya Nandagala, Wilaya ya Ruangwa.


Sherehe hiyo iliyolenga kuwaaga Wajumbe hao kwa kipindi cha utumishi wao, imehudhuriwa na wageni mbalimbali kutoka Kata ya Nandagala, akiwemo Chifu wa Wilaya ya Ruangwa, Mzee Said Mohamed Chipenye, Mwenyekiti wa Wenyeviti Wilaya ya Ruangwa Mhe. Garus Nnunduma, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa (Diwani wa Kata ya Nandagala) Mhe. Andrew Chikongwe, ambaye amekuwa mgeni rasmi wa hafla hiyo.


Aidha, Wajumbe hao wametumia fursa hiyo kupongezana kwa mafanikio makubwa ya maendeleo waliyoleta ndani ya Kata yao katika kipindi cha miaka mitano ya utumishi wao, kuanzia mwaka 2019 hadi 2024. Wameeleza furaha yao kuwa sherehe hiyo imefana sana, huku wakiweka wazi kuwa ni mara ya kwanza kwa Wajumbe kujipongeza kwa utumishi bora ndani ya Kata ya Nandagala.


Mbali na hayo, Wataalamu wa Kilimo na Elimu wa kata hiyo wametoa shukrani zao kwa maendeleo makubwa yaliyopatikana katika sekta za Kilimo na Elimu, ikiwa ni pamoja na miradi mikubwa ya kilimo cha umwagiliaji na maendeleo ya elimu yaliyopatikana kwa kipindi cha miaka mitano. Kwa moyo wa dhati, wameipongeza Serikali kwa juhudi zake za kuchapa kazi na kuleta maendeleo kwa wananchi.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Garus Nnunduma, amewasisitiza Wajumbe wa Serikali za Vijiji kuzitendea haki nyadhifa walizopewa. Amesema, “Sherehe hii iwe chachu ya kujitathmini na kuzipima kazi mlizozifanya ndani ya miaka mitano, lakini pia iwaoneshe namna mnavyopaswa kuwajibika kwa ajili ya wananchi wenu. Ukipewa dhamana ya kuwatumikia wananchi, wajibika ipasavyo na siyo kuwa mtu wa kubisha na kupinga kila jambo.”


Naye, Chifu wa Wilaya ya Ruangwa, Mzee Said Mohamed Chipenye, amesema, “Uongozi bora unaanzia kwenye kujitambua na kuheshimu mila na desturi zetu, tunapoendelea na maendeleo ni muhimu kuhakikisha kwamba tunadumisha utamaduni wetu na kuendeleza maadili bora kwa kizazi kijacho.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa