• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

RUANGWA TUPO NANE NANE NGONGO

Posted on: August 4th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa inashiriki Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini, yanayofanyika katika viwanja vya Ngongo vilivyopo Manispaa ya Lindi, maonesho yameanza rasmi tarehe 1 Agosti 2024 na kilele chake ni tarehe 8 Agosti 2024, ikumbukwe, manesho ya Nanenane yanatoa fursa kwa wananchi kujifunza na kuelewa teknolojia mpya zinazohusiana na kilimo, uvuvi, na ufugaji wa kisasa.


Hii ni fursa adhimu kwa wakulima, wafugaji, na wavuvi kuja kujifunza kuhusu mbinu bora na teknolojia za kisasa ambazo zinaweza kuboresha uzalishaji na kuongeza kipato. Huduma zitolewazo ni; Elimu ya upimaji afya ya udongo, Elimu ya matumizi bora ya mbolea, Elimu ya Mfumo wa M-KILIMO huu ni mfumo unaotoa huduma za ugani na masoko kupitia simu ya mkononi. Pia, maonesho haya yanatoa nafasi ya kuonyesha bidhaa mbalimbali na kujifunza kutoka kwa wataalam katika sekta husika.


Ikumbukwe, Maonesho ya Nanenane yalianza rasmi mwaka 1993 na yanaratibiwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali. Tukio hili la kitaifa linalenga kuhamasisha maendeleo katika sekta za kilimo, mifugo, na uvuvi. Kila mwaka, maonesho haya huandaliwa katika kanda tofauti nchini, ambapo wakulima na wadau wanapata nafasi ya kubadilishana uzoefu na kupata maarifa mapya. Maonesho haya yamekuwa yakifanyika kwa mafanikio na ni sehemu muhimu ya kalenda ya kilimo nchini.


Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi." Kauli mbiu hii inasisitiza umuhimu wa kuchagua viongozi wenye uwezo wa kuleta maendeleo endelevu katika sekta hizi muhimu za uchumi.


Tunawakaribisha kwa wingi kutembelea banda letu ili kupata maarifa muhimu ambayo yatasaidia kuboresha shughuli za uzalishaji. Pamoja, tutaweza kujifunza, kubadilishana mawazo, na kujadili mbinu bora za kuboresha ustawi wa jamii yetu. Karibu sana!

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa