• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Pro. Mbalawa aagiza kusimamishwa kwa mkandarasi wa maji narungombe

Posted on: September 26th, 2019

Waziri wa Maji Nchini Prof. Makame Mbalawa ameagiza kusimamishwa kwa Mkandarasi anaeshughulika na ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Narungombe Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi kutokana na mkandarasi huyo kutumia muda mrefu kutekeleza mradi huo ilhali alishalipwa awamu ya kwanza aliyostahili na kutakiwa kukamilisha mradi tokea mwezi februari mwaka huu.

Mhandisi huyo anaefahamika kwa jina la Waziri Jabiri wa kampuni ya SYSCON BUILDERS LTD,  amechukuliwa hatua hiyo na prof. Mbalawa septemba 26 mwaka huu alipokuwa katika ziara yake ya kikazi Wilayani humo ambapo alifika katika kijiji cha Narungombe ambako kampuni hiyo   ilipewa kandarasi  kujenga mradi wa maji kijijini hapo kuonekana kutomaliza mradi kwa wakati licha ya mhandisi wa kampuni hiyo  kukiri kupokea fedha za kazi hiyo na kutoitekeleza kwa wakati.


“kesho muanze taratibu za kumsimamisha Mhandisi huyo na mtupatie wenyewe tufanye kazi, hatuwezi kukaa na kuangalia wananchi wetu wanateseka na mimi siwezi kuja hapa kupiga maneno kila siku nikaonekana ni muongo, wakati naamini tukichukua sisi mradi ndani ya mwezi mmoja na nusu tunaumaliza kwa nini tukupe wewe wakati tushakupa muda na haukumaliza? ” alisema Prof. Mbalawa, alipokuwa akimhoji mhandisi Jabiri aliepewa kandarasi hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti  wa Halmashauri ya Wilaya ya  Ruangwa Rashidi  Nakumbiya amepongeza maamuzi hayo ya Waziri kutokana na haja kuwa wananchi wamekua wakihitaji maji kwa muda mrefu bila mafanikio kutokana na uzembe wa mkandarasi huyo.

“haya malalamiko ya mradi kuchelewa wananchi wanayajua na wamelalamika kwa muda mrefu na wamepata hii tabu kwa muda mrefu, ilikua ndio kwa mara ya kwanza wenzetu hawa wapate maji lakini mwenzetu ambae alipaswa kushughulikia hili jambo ametuangusha hatua ulioichukua Mheshimiwa Mbalawa ni muafaka na kwa wakati muafaka ili kuweza kuokoa na kurudisha matumaini ya wananchi kwa serikali yao lakini pia kuondokana na tatizo la maji limekua ndoto zao kwa muda mrefu sana” alisema Mh. Nakumbya.

Baaadhi  ya wananchi wakiwemo zaudia mjogo na Rashidi salumu  wamesema wamekua wakipata tabu ya kujihimuu usiku wa saa tisa kufuata maji yaliko ili kuwahi foleni na wakati mwingine kupelekea kushinda huko siku nzima bila mafanikio na hivyo kusema kuwa kukamilika kwa mradi huo kunaweza kuja kuwakomboa na hadha hiyo ambayo wamekua wakiipata kwa miaka mingi sasa.

“tunashida ya maji hii tabu ni ya muda mrefu, tumeomba msaada toka muda mrefu, hatulali tunakesha maporini kwenye vyanzo vya maji kutafuta maji” alisema Zaudia majogo ambae ni mkazi wa Narungombe.

Mradi  wa maji katika kijiji cha narungombe unagaharimu Shilingi milioni 300 huku zaidi ya milioni 100 zikiwa ameshalipwa mkandarasi huyo lakini bado utekelezaji wake umekua wa kusua sua jambo lilopelekea kusimamishwa kwa kandarasi yake.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa