• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

PPRA YATOA MAFUNZO YA MFUMO WA NeST RUANGWA

Posted on: April 14th, 2025


Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Kusini imeendesha mafunzo maalum kwa viongozi wa taasisi za umma, yakiwemo mashule na vituo vya afya, ili kuwajengea uwezo wa kutumia mfumo wa kielektroniki wa usimamizi wa ununuzi wa umma ujulikanao kama NeST.


Mafunzo hayo yamefanyika Aprili 14, 2025 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nkowe yamehusisha Waganga Wafawidhi, Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu pamoja na Walimu wa Manunuzi, ambapo walifundishwa kuhusu matumizi sahihi ya mfumo huo kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma Na. 10 ya mwaka 2023 na Kanuni za mwaka 2024.


Akizungumza na washiriki, Afisa Manunuzi Mwandamizi wa PPRA Kanda ya Kusini, Mtaka Membe, amesema baadhi ya taasisi za umma katika ngazi ya msingi zimekuwa zikitumia fedha za serikali bila kufuata miongozo ya manunuzi, hali inayochangia kupotea kwa rasilimali na kuathiri uwajibikaji.


“NeST ni mfumo uliobuniwa kulinda fedha za umma kwa kuhakikisha uwazi, ushindani wa haki, na thamani halisi ya fedha katika kila hatua ya mchakato wa manunuzi,” amesema Membe wakati wa mafunzo hayo.


Taarifa kutoka PPRA zinaeleza kuwa mfumo wa NeST unajumuisha hatua zote kuanzia maandalizi ya mpango wa ununuzi, uandaaji na tathmini ya zabuni, utoaji wa tuzo, hadi usimamizi wa mikataba kwa njia ya kidijitali.


Mbali na hayo, washiriki walielimishwa kuhusu majukumu ya wadau mbalimbali wa manunuzi ndani ya taasisi zao, wakiwemo Maafisa Masuuli, Maafisa Manunuzi, Idara tumizi pamoja na Kamati za Zabuni ili kuhakikisha kila hatua ya ununuzi inatekelezwa kwa weledi.


Baadhi ya washiriki wa mafunzo wamepongeza juhudi za PPRA, wakisema elimu waliyoipata itawasaidia kuboresha usimamizi wa rasilimali na kutumia mfumo wa NeST kwa ufanisi ili kuepuka ukiukwaji wa taratibu za kisheria.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa