• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Pongezi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

Posted on: March 12th, 2018

Kamati ya  Fedha, Uongozi  na Mipango imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kubuni chanzo cha mapato ambacho ni shamba la mikorosho litakalokuwa linamilikiwa na Halmashauri hiyo.

Hayo yamesemwa na kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango katika shamba la miche ya mikorosho lililopo vijiji vya Machang’anja na Nangurugai baada ya kufanya ziara yake machi 12/2018.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Rashidi Nakumbya aliupongeza uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kazi kubwa iliyofanyika ya kusafisha na kuanza kupanda miche hiyo ya mikorosho.

“Kazi imefanyika kubwa na inaonekana kilichobaki sasa ni kukimbizana na kipindi hiki cha mvua mpande miche iliyobaki, mjitahidi mpaka wiki inayokuja muwe mmemaliza shughuli za upandaji”amesema Nakumbya

Aidha Mheshimiwa Nakumbya amesema wananchi waliopo katika eneo la shamba la Halmashauri ni watu wanaowategemea katika uangalizi wa shamba kwa kipindi hiki na kuwaomba kuwa wavumilivu wakati wanawaangali jinsi ya kutatua malalamiko yao

“Nyie ni watu muhimu sana hatuwezi kuwaacha mnanung’unika sisi kama wanakamati hii tutalichukua jambo hili na kulizungumzia sehemu husika, ila wakati mnaendelea na uchimbaji wa mashimo ya kupanda miche ya mikorosho ule ufuta mliopanda wa kule bondeni mjitahidi kuung’olea usije ukaharibika” amesema Nakumbya.

Naye Afisa Kilimo wa Wilaya Haronii Kihara alilielezea shamba hilo kwa kamati kuwa ni mkakati wa muda mrefu wa kuongeza mapato kwa halmashauri.

Kihara amesema shamba hilo linaukubwa wa ekari 1,000 ambalo halmashauri imepanga kupanda miche ya mikorosho ambayo itakuwa tayari kuvuna baada ya miaka 2.

Aliendelea kusema kutokana na ukubwa wa shamba Halmashauri imepanga kupanda ekari elf 200 kwa mwaka 2018, ambapo kila ekari moja itakuwa na miche 68 na kila mche utatoa kilo tatu za korosho wakati wa mavuno.

“Waheshimiwa Madiwani ufuta mnaouona sasa shambani hapa si wa Halmashauri bali ni wa wakulima ambao tumewapa maeneo haya bure walime kwa makubaliano ya kutulindia shamba hili hata nyie waheshimiwa mnakaribishwa kuja kulima” amesema kihara

Halmashauri imesafisha shamba kwa gharama zake ila inakaribisha wakulima kuja kulima eneo hilo ili waweze kulinda miche iliyopo shambani hapo na pia Halmashauri imetoa ajira kwani wakulima wanaolima katika eneo hilo wamepata kibarua cha kuchimba mashimo na kupanda miche.

Naye Mkulima wa Ufuta Omari Saidi aliuomba uongozi wa Halmashauri waanze kuchimba mashimo katika maeneo waliolima ufuta kabla ufuta aujajifunga na waliomba mashimo ya miche katika maeneo waliolima wapande wenyewe kwa ajili ya kutunza walichilima.

“Tunakaribia kuondoka kurudi majumbani kwetu hivyo tunaomba mashimo yaanzwe kuchimbwa huku kwenye mashamba yetu ya ufuta na tuchimbe wenyewe wasije watu wengine wakaharibu” amesema Omari.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa