• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MWENYEKITI WA HALMASHAURI AFANYA ZIARA YA KUWATEMBELEA WAFUGAJI KUKU KATA YA NANDAGALA

Posted on: July 14th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Andrew Chikongwe amefanya ziara ya kuwatembelea wafugaji wa kuku kutoka kijiji cha Nandagala wilayani Ruangwa ambao ni wanufaika wa mradi wa TPGS akiambatana na Daktari wa Mifugo Kata ya Nandagala pamoja na Mtendaji Kata ya Nandagala.


Ziara hiyo ameifanya leo Julai 14, 2024 ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa wanufaika wa mradi huo namna gani bora ya kufuga na faida zake na kutoa wito kwa wafugaji hao kuzingatia namna bora ya ufugaji kwani soko la kuku wa nyama na mayai halijawahi kujaa.


" Mimi niwaambie tu yakwamba hili jambo si dogo na lina manufaa makubwa sana kwenu, soko la kuku wa nyama na mayai halijawahi kujaa, wahitaji ni wengi sana endapo mutazingatia vizuri ufugaji huu, msidharau kabisa au kuishi kwa kitegemea kilimo tu hata ufugaji pia una manufaa kwetu" Amesema Chikongwe.


Mradi wa Tropical Poutry Genetics Solution (TPGS) una lengo la kuendeleza kizazi cha kuku na kuifundisha jamii namna gani nzuri ya kufuga kuku kwa maendeleo endelevu katika familia.


Ili kuendeleza kizazi cha kuku TPGS ina Kituo kikubwa cha chanjo za Mifugo ambapo kipo Arusha na kwa Kanda ya Kusini kipo kituo cha utafiti wa Mifugo Naliendele, Mtwara.


Kwa upande wao wafugaji wa kuku kutoka kijiji cha Nandagala walionufaika na Mradi huo, waliopata kuku 25 wapo nane, waliopata kuku 50 wapo nane na waliopata kuku 75 wapo nane na kufanya jumla ya watu 24 waliopatiwa kuku aina ya Saso na Tanbrow Juni 6, 2024.


Kuku aina ya Saso na Tanbrow wana uwezo wa kutaga mayai 270 - 300 kwa kila kuku mmoja kwa mwaka na ukomo wa kutaga mayai ni miaka miwili.


Kwa upande wake, Daktari wa Mifugo Kata ya Nandagala Jenifer Moses amesema ili kudumisha ufugaji wa kuku kuna haja ya kuwa na Kituo cha utafiti wilayani Ruangwa kwasababu itasaidia kupunguza gharama kwa mfugaji endapo mfugo utapata homa na kuhitajika kufanyiwa uchunguzi zaidi.


Naye, Mtendaji wa Kata ya Nandagala Bi Awesa Rashidi ametoa wito kwa wananchi kufuga kwa kuzingatia kanuni bora za ufugaji wa kuku na kuendeleza ufugaji huo kwani ni mtaji katika familia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa