• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKULIMA AKIKWAMULIWA , NA TAASISI ZA KIFEDHA ZINAJIKWAMUA KIUCHUMI

Posted on: July 12th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Andrew Chikongwe ametoa wito kwa Taasisi ya fedha, Benki ya NMB tawi la Ruangwa kumwezesha mkulima katika nyenzo kwani mkulima akikwamuliwa basi inasaidia hata Benki hiyo kujikwamua kiuchumi.


"Watu wapo tayari kwa kilimo, lakini wanakosa nyenzo, hivyo basi nikuombe Meneja wa Benki ya NMB kuwasaidia wakulima hawa kupata nyenzo zitakazowasaidia kuongeza kasi ya uzalishaji na wewe ni mwenzetu na tuna imani kubwa sana na wewe ya kwamba utatukwamua katika hili" Amesema Chikongwe.


Ameyasema hayo leo Julai 12, 2024 katika Kikao kilichofanyika katika Kijiji cha Namahema B kilichopo Kata ya Nandagala wilayani Ruangwa.


Kikao hicho kilihusisha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Viongozi wa Kata ya Nandagala, Viongozi wa kijiji cha Namahema B, Viongozi wa Benki ya NMB, na wakulima wa bustani za mbogamboga wa Kata ya Nandagala na Mnacho.


Pia, Kikao kilihusisha kutembelea wakulima wa bustani za mbogamboga akiwemo Ndugu Mohamed Said Chipenya ambaye anajihusisha na kilimo hicho kwa umwagiliaji wa mkono (mashilingwete), Imamu Abeid pamoja na Mussa Nassoro ambao hutumia njia za kisasa katika kilimo hicho cha mbogamboga na kuona utofauti mkubwa uliopo kati ya mkulima ambaye hutumia njia zisizo za kisasa na yule ambaye hutumia njia za kisasa katika kilimo hicho.


Kwa upande wake Meneja wa Benki ya NMB tawi la Ruangwa Ndugu Habibu Moris amesema nia wanayo ya kuwasaidia wakulima kwa sababu kupitia ziara ya kuwatembelea wakulima wamejifunza mengi lakini uaminifu ni silaha kubwa sana katika kufanikisha hayo yote.


" Ni kweli mkulima akikwamuliwa na sisi tunakuwa tumejikwamua kwasababu Benki kazi yake ni kuhifadhi akiba za watu, na kutoa mikopo kwa watu, hivyo tunavyoamua kuwakopesha na nyie muoneshe uaminifu kwa kurejesha mikopo kwa wakati ili kuendelea kufanya kazi kwa weredi kama Taasisi, usivyorudisha kwa wakati wengine wanakosa huduma" Amesema Moris


Kijiji cha Namahema B kina jumla ya wakulima 215 ambapo wakulima wa mbogamboga ni 86, wakulima wa Korosho ni 40 na wakulima wa mazao ya chakula ni 89.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa