• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Mhe, Mwenyekiti Wa Halmashauri Amawataka Kina Mama Wajawazito Kujitokeza Kwa Wingi Kuunganishwa Katika Fao La Tumaini La Mama

Posted on: May 26th, 2017

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ruangwa Rashidi Nakumbya amewataka wahudumu wa afya kufanya hamasa kwa wamama wajawazito ili waweze kuingizwa katika mpango wa tumaini la mama.

Alisema kufanya hivyo itasaidia sana kupunguza idadi ya vifo vya wakina mama na watoto wachanga kwani watakuwa wamepata huduma mapema na mtoto ataendelea kupata huduma bora na bure kwa muda wote wa ujauzito.

Aliyasema hayo wakati akiongea na wahudumu wa afya waliohudhuria kwenye mafunzo yaliyotolewa na Ofisi ya Bima ya Afya Mkoa, alitumia nafasi hiyo kuishukuru Ofisi ya Bima ya Afya Mkoa na Benki ya serikali ya Ujerumani.


Aidha Mhe. Nakumbya aliwaasa wahudumu wa afya kuwa na lugha nzuri za kuzungumza na wateja pale wanapoitaji huduma, kwani hii itasaidia kuwepo na ukaribu wa mgonjwa na mtoa hudumu.

Mhe. Mwenyekiti alisema kuwa kuna changamoto nyingi ambazo watumishi wa afya hukutana nazo maeneo yao ya kazi, hata hivyo hawapaswi kukata tamaa bali kuzifanya changamoto hizo kuwa ni fursa ili kufikia malengo mazuri ya kumaliza vifo vya watoto na wazazi.


Naye Meneja wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa Bwana Emmanuel, Mwikwabe alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwasaidia watanzania kupata huduma za afya kwa urahisi kupitia bima, alisisitiza gharama za matibabu ni kubwa bila bima ya afya ni vingumu kila mwananchi kupata huduma anazoziitaji.

Aliwataka wahudumu wa afya kujitahidi kutumia nafasi hii iliyopatikana kuwasajili akinamama kwa wingi na kutoa elimu ya bima ya afya kwa wateja wao, ikitokea jamii ikatambua umuhimu wa bima ya afya wananchi watapiga hatua katika maendeleo ya jamii.


Naye Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Japhet Simeo aliwataka watumishi wa afya kuwatumia wahudumu wa afya kwa ngazi ya vijiji kwani wao ni rahisi kuwabaini akina mama wajawazito kwenye maeneo yao.

Tumaini la mama ni fao linalotolewa na Mfuko wa Bima ya Afya.Fao hili linafadhiliwa na benki ya wananchi wa ujerumani, lengo kuu la fao hili ni kuboresha afya ya mama mjamzito na miezi 6 baada ya kujifungua. Pia kuboresha upatikanaji wa dawa,vitendanishi na vifaa tiba. Halikadhalika Fao hili litasaidia kuboresha Miundombinu ya kutolea huduma


Tumaini la mama ni fao ambalo mama yoyote mjamzito husajiliwa na kupewa namba ya utambulisho ambayo huandikwa kwenye kadi yake ya kliniki na kumruhusu kutibiwa mahali popote ndani ya Mkoa

Vile vile fao limetoa fursa ya kuwalipia kadi za (CHF) wanafamilia wa mama wajawazito kwa mwaka mmoja, wanufaika hawa wa CHF hutibiwa ndani ya Halmashauri husika.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa