• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MHE. CHIKONGWE AWATAKA WANANCHI WA RUANGWA KUENDELEZA USAFI, KILIMO CHA KISASA NA KUJALI AFYA

Posted on: April 16th, 2025




Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Andrew Chikongwe, amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kuendeleza utamaduni wa kufanya usafi wa mazingira, kuwekeza katika kilimo cha kisasa, na kujali afya zao, akisema afya bora ni msingi wa maendeleo ya mtu binafsi na jamii kwa ujumla.


Wito huo umetolewa leo Aprili 16, 2025, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mbekenyera, ambapo viongozi mbalimbali wa kata, wajumbe wa Serikali za Vijiji, vikundi vya wanufaika wa mikopo, pamoja na wananchi wamehudhuria na kujadili namna ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii.


Aidha, Mhe. Chikongwe amesema maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila wananchi kuwa na afya njema, mazingira safi na kushiriki kwenye shughuli za uzalishaji mali kama kilimo.


“Tukijenga haya matatu kwa pamoja usafi wa mazingira, kilimo cha kisasa na afya bora tutakuwa tumejenga msingi wa maendeleo endelevu,” amesema Mhe. Chikongwe.


Sambamba na hayo, ametoa wito kwa wanufaika wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kuhakikisha wanazitumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kujikwamua kiuchumi, akisisitiza kwamba Fedha hizo si kwa matumizi binafsi wala za anasa, bali ni mtaji wa maendeleo, wazitumie kwa umakini ili zitengeneze matokeo chanya.


Katika hatua nyingine, amewahimiza wazazi kuwa na ushirikiano wa karibu na walimu kwa kufuatilia maendeleo ya watoto wao badala ya kuwaachia walimu jukumu hilo pekee. “Wazazi mnapaswa kushirikiana na walimu ili kuhakikisha watoto wetu wanafanya vizuri. Malezi na elimu ni jukumu la pamoja,” amesisitiza.


Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mbekenyera, Mhe. Hamis Chimale, ameunga mkono kauli hiyo ya Mwenyekiti na kuwataka wananchi kuyafanyia kazi maelekezo yaliyotolewa ili kuleta maendeleo kwa wote.


Naye Mohammed Kassim, ambaye amezungumza kwa niaba ya wananchi waliohudhuria mkutano huo, ameushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kuandaa mkutano na kutoa elimu kwa jamii.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa