• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAONESHO YA 31 YA NANE NANE KANDA YA KUSINI YATAMATIKA

Posted on: August 8th, 2024

Maonesho ya 31 ya Nanenane Kanda ya Kusini yametamatika leo 8 Agosti 2024 kwa mafanikio makubwa, yakionesha maendeleo ya sekta ya kilimo, ufugaji, na uvuvi katika Mikoa ya Lindi na Mtwara. Maonesho hayo, ambayo yamefanyika kwa siku nane katika viwanja vya Ngongo, Lindi, yamehudhuriwa na maelfu ya wakulima, wafugaji, wavuvi, na wadau mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali ya kanda ya kusini na nje ya kanda hiyo.


Katika hotuba yake ya kufunga maonesho hayo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Ikulu (kazi maalum), Mhe. George H. Mkuchika, amepongeza jitihada za wakulima na wadau wa sekta ya kilimo katika kuongeza uzalishaji na ubunifu. Amesema maonesho ya mwaka huu yameweka rekodi mpya kwa kuonesha teknolojia za kisasa zaidi zinazoweza kuboresha uzalishaji na kuongeza tija katika sekta ya kilimo.


Aidha, Mhe. Mkuchika amewaimiza wakulima kufanya shughuli zao za kilimo kwa bidii maana kilimo ni uti wa mgongo amewaomba kutumia vizuri elimu walizopatiwa kwenye maonesho ya 31 ya Nanenane kanda ya kusini 2024 ili kufanya kilimo chenye tija na manufaa kwao na kwa Taifa kwa ujumla.


Sambamba na hayo, Mhe. Mkuchika amesisitiza Wananchi wote wenye sifa kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa lakini pia, wasiache kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kutimiza takwa lao la kikatiba la kuchagua viongozi wao.


Mbali na hayo, zawadi kwa makundi mbalimbali yaliyofanya vizuri zimetolewa kwenye maonesho hayo ikiwa ni sehemu ya motisha na kujali juhudi na jitihada za wadau wa kilimo, mifugo na uvuvi.


Ikumbukwe, Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kujifunza teknolojia mpya, na kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya kilimo, ufugaji, na uvuvi. Serikali imeahidi kuendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kuwa maonesho haya yanaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa kanda ya kusini na Tanzania kwa ujumla. Mwaka ujao, maonesho haya yanatarajiwa kuwa na mwitikio mkubwa zaidi, huku serikali ikiahidi kuongeza ushiriki wa wanawake na vijana katika sekta ya kilimo na ufugaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa