• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAFUNZO YA KIKAO KAZI CHA WATAALAMU LINDI JUU YA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA YAFANYIKA RUANGWA

Posted on: February 18th, 2025

Wizara ya Katiba na Sheria imefanya kikao kazi na wataalamu kuelekea uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mkoa wa Lindi, Kikao hicho kimefanyika leo Februari 18, 2025, katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, kikiwaleta pamoja Maafisa Maendeleo ya Jamii, Maafisa Ustawi wa Jamii, Wanasheria, Maafisa Habari, Wapima Ardhi, Wasajili na Polisi kutoka Dawati la Jinsia.


Kampeni hiyo inalenga kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu haki zao za kisheria na kuwapatia msaada wa sheria bure, hususan kwa wanawake, watoto, na makundi mengine yenye uhitaji na inatarajiwa kusaidia kutatua migogoro ya ardhi, ndoa, mirathi, na masuala mengine ya haki za binadamu, huku ikitekelezwa katika Mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar kwa awamu.


Aidha, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Nathalis Linuma, ambaye amefungua kikao kazi hicho, amesema wataalamu wa sheria wanapaswa kushirikiana kwa karibu na jamii ili kuhakikisha elimu ya msaada wa kisheria inawafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati muafaka.


Naye, Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Esther Msambazi, amesema uzinduzi rasmi wa kampeni hiyo utafanyika Februari 19, 2025, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.


Ameongeza kuwa kampeni hiyo tayari imefika katika mikoa 17 na imeonyesha mafanikio makubwa kwa kuwawezesha wananchi kupata msaada wa kisheria na kutatua migogoro mbalimbali. Malengo ya kampeni hiyo ni kufikia mikoa 26 ya Tanzania Bara na mikoa 5 ya Zanzibar ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wananufaika na huduma hizo.


Kwa upande wake, Mtaalamu wa Ardhi, Andrew Munisi, amesema watahakikisha wananchi wanapata msaada wa kisheria katika utatuzi wa migogoro ya ardhi, huku Mkuu wa Dawati la Jinsia Mkoa wa Lindi, Joyce Kitesho, akisisitiza kuwa kampeni hiyo ni nyenzo muhimu ya kusaidia wanawake na watoto waliokumbwa na changamoto za kisheria.


Kwa miaka ya nyuma, wananchi wengi wamekuwa na uelewa mdogo kuhusu haki zao za kisheria, hali iliyopelekea ongezeko la migogoro na manyanyaso, hata hivyo, kupitia kampeni hii, Serikali imeongeza mwamko wa wananchi juu ya haki zao. Hatua inayofuata ni kuhakikisha elimu hii inawafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati sahihi.


Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia imebeba kauli mbiu “Msaada wa Kisheria kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo,”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa