• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MAAFISA MAENDELEO NGAZI YA KATA WAPEWA MAFUNZO YA USIMAMIZI WA MIKOPO 10% RUANGWA

Posted on: October 1st, 2024

Maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata wamepewa mafunzo kuhusu usimamizi na utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana, na walemavu mafunzo hayo yamefanyika leo, Oktoba 1, 2024, katika ukumbi wa Ofisi ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa. 



Mafunzo hayo yamehusisha maafisa maendeleo ya jamii kutoka kata zote 22 za Wilaya ya Ruangwa yakiwa na lengo la kuimarisha uelewa kuhusu mikakati ya usimamizi wa maendeleo ya jamii, hususani katika kusimamia mikopo ya 10% kwa kufuata taratibu zote zinazotakiwa.


Aidha, mafunzo yameendeshwa na Maafisa maendeleo ya Jamii ngazi ya Wilaya wakiongozwa na ndugu Rashid Namkulala, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Ruangwa, ambapo Ndugu Namkulala amesisitiza umuhimu wa mikopo hiyo katika kuboresha maisha ya wanajamii, huku akiwataka maafisa hao kuyazingatia mafunzo ili kuboresha zaidi utenda kazi wao katika kusimamia mikopo hiyo.


 "Mikopo hii inatoa fursa kwa vikundi vya wanawake, vijana, na walemavu kujiendeleza kiuchumi na hivyo kuchangia katika maendeleo ya jamii nzima, ni matumaini yangu kwamba mafunzo haya wataongeza mara dufu utenda kazi wenu na pia yatasaidia kuleta mabadiliko chanya." Amesema Namkulala. 


Sambamba na hayo, mafunzo hayo yameletwa wakati ambapo kuna umuhimu mkubwa wa kuimarisha ushirikiano kati ya Halmashauri na vikundi vya maendeleo. Washiriki wamepata nafasi ya kujifunza kuhusu taratibu za kuandika maombi ya mikopo, pamoja na jinsi ya kusimamia fedha hizo kwa ufanisi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa, hii inatarajiwa kuongeza ufanisi katika matumizi ya rasilimali.


Mbali na hayo, katika kipindi cha mafunzo, washiriki wamehusishwa moja kwa moja katika mijadala, ambapo wameweza kutoa mawazo na maswali kuhusu usimamizi wa mikopo hiyo, pia yametoa fursa ya kubadilishana uzoefu na kukuza mbinu bora za kazi.


Ikumbukwe, Maafisa maendeleo ya jamii wamehimizwa kuendeleza elimu waliyoipata kwa vikundi vyao ili kuhakikisha rasilimali zinatumika ipasavyo na kusaidia katika kuboresha maisha ya jamii. Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa inaamini kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu ya mabadiliko chanya katika maendeleo ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MAAFISA WAANDIKISHAJI WAPEWA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU RUANGWA

    May 14, 2025
  • CHONYA AWATAKA MAAFISA WAANDIKISHAJI RUANGWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU

    May 14, 2025
  • CHONYA AWATAKA MAAFISA WAANDIKISHAJI RUANGWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU

    May 14, 2025
  • KUWEKWA WAZI DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    May 13, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa