• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Kikao cha Wadau wa Elimu

Posted on: February 21st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi ameitisha kikao cha wadau wa elimu wilaya ya Ruangwa ili kujadili namna gani wilaya inapanda kiufaulu kwa mitihani ya taifa ya shule za msingi na sekondari tofauti na hali mbaya ya ufaulu iliyopo sasa.

Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Narung’ombe uliopo Ruangwa mjini na uliwashirikisha Walimu, wenyeviti wa kamati na bodi za shule, maafisa elimu kata, madiwani, wenyeviti wa vijiji, viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya siasa, wazee maarufu na wazazi.

Mhe. Zambi alisema kuwa mkoa kiufaulu upo chini sana ambapo kwa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ulikuwa wa 27 na kwa upande wa shule za msingi ulikuwa wa 14.

Katika majadiliano mdau wa Elimu Mheshimiwa Diwani Elias Nkane alisema ni lazima kuwe na ushirikiano baina ya walimu na waratibu elimu, madiwani, wazazi na viongozi wote katika wilaya katika kusimamia maendeleo ya elimu.

Aidha, Damares Namlehu alisema kumekuwa na tabia ya baadhi wazazi kutekeleza watoto wao bila sababu za msingi ambapo ameiomba serikali kuwachukulia hatua wazazi wenye tabia hizi na wale wanaofanya kilimo cha kuhamahama ambacho kinapelekea utoro mashuleni.

Naye Issa Mmaka amesema tatizo jingine ni ukosefe wa walimu wa sayansi na hisabati katika shule na kusababisha watoto kufanya vibaya kwenye mitihani ya masomo hayo.

Chilemba Daniel amesema maafisa elimu msingi na sekondari wapite katika kila shule kufuatilia mara kwa mara maendeleo ya wanafunzi na walimu. Pia alishauri lugha ya kingereza ufundishwaji wake usimamiwe kuanzia darasa la tatu.

Naye Hassan Snola amesema wazazi wanatakiwa kuacha kuingilia majukumu ya walimu kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha walimu kukatatamaa na kushindwa kufanya kazi kama inavyotakiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Joseph Mkirikiti amewataka watu kuacha kukaa vijiweni, maana wanafunzi wanaotoroka shule wanaenda kwenye vijiwe hivyo kuanzia sasa kutakuwa na operationi maalamu ya watu wanaokaa vijiweni.

“Niwaagize watendaji wa kata na vijiji kuanzia kesho kupita katika vijiwe, vibanda vya sinema na maeneo mengine kuwakamata watoto watoro na kuhakikisha mnawachukulia hatua kali wamiliki wa vibanda vya video wanao waruhusu wanafunzi kuingia humo badala ya kusoma”, amesema Mhe. Mkirikiti.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa alishauri wazazi kupitia kamati na bodi za shule kuona umuhimu wa kuchangia chakula katika shule kwa kufuata utaratibu ili kuondoa changamoto iliyopo ya watoto kukaa na njaa muda mrefu hali inayoondoa usikivu wa masomo ipasavyo.

“Suala la kuchangia chakula ni hiyari ya mzazi halazimiswi ila sisi kama serikali tunawaeleza umuhimu wa chakula kwa wanafunzi wanapokuwa shuleni na nimeshaelekeza kuwa mwanafunzi ambaye mzazi wake ataki kuchangia chakula asifukuzwe badala yake ukifika muda wa chakula huyo mtoto asipewe chakula.”, amesema Mhe. Zambi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa