• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

KATA YA NACHINGWEA YAONGOZA KUWA NA IDADI KUBWA YA WATU WILAYANI RUANGWA

Posted on: July 2nd, 2024

Kwa mujibu wa Takwimu za Matokeo ya Sensa ya watu na makazi 2022 Kata ya Nachingwea wilayani Ruangwa inaongoza kuwa na idadi ya watu wengi ikiwa na watu 18,343 ikifuatiwa na Kata ya Mbekenyera yenye watu 16,531, Kata ya Nandagala ikiwa na watu 7391, huku Kata ya mwisho ikiwa ni Makanjiro yenye watu 4002 na kufanya Wilaya ya Ruangwa kuwa na julma ya watu 185,573.


Aidha, Matokeo ya Sensa ya watu na makazi imeonesha uwiano wa watu kwa jinsia idadi ya Wanaume kwa kila Wanawake 100 ambapo kwa Wilaya ya Ruangwa ina uwiano ya Wanaume 97 kwa kila Wanawake 100.


Na katika Kata za Wilaya ya Ruangwa Kata inayoongoza kwa kuwa uwiano wa juu wa jinsia kati ya Wanaume na Wanawake ni Kata ya Mbwemkuru, Machang'anja,Nambilanje, Mbekenyera, Matambarare na Chibula na hii inaonesha kwamba Wanaume ni wengi kuliko Wanawake.


Kata ya Namichiga na Chienjele uwiano wa jinsia kati ya Wanaume na Wanawake ni 100 kwa 100 na Kata ya Nandagala uwiano wa jinsia ni Wanaume 93 kwa Wanawake 100, na Kata ya Mnacho ina uwiano mdogo wa watu kwa jinsia kwa kuwa na Wanaume 91 kwa Wanawake 100.


Katika upande wa Idadi ya Kaya katika Wilaya ya Ruangwa ina jumla ya Kaya 60931 na Kata ambayo inaongoza kwa idadi kubwa ya Kaya ni Kata ya Nambilanje ambayo inaongoza kwa wastani mkubwa wa watu kwa Kaya ina wastani wa watu 3.5, Mbwemkuru wastani wa watu 3.3, Nandagala wastani wa watu 3.0 na Mnacho wastani wa watu 2.8.


Sensa ya watu na makazi 2022 aidha imeonesha idadi ya watoto chini ya umri wa miaka 18 ambapo kwa Wilaya ya Ruangwa ina 37% ya watoto chini ya miaka 18.


Na Kata inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watoto chini ya miaka 18 ni Kata ya Nambilanje 40.3%, Mbwemkuru 40.0%, Nandagala ina 35.6%, na Mbekenyera ina 34.4%.


Takwimu za idadi ya Vijana kuanzia umri wa miaka 15-35 katika Wilaya ya Ruangwa ni 34.6% ambapo Kata ya Nachingwea inaongoza kuwa na vijana wengi zaidi ya 40.9%, Mbekenyera ni 38.5%, Nandagala ni 33.6% na Malolo ina asilimia ndogo ya Vijana ambayo ni 30.4 ukilinganisha na Kata zote wilayani humo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa