• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

KALIUA YAJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI RUANGWA

Posted on: December 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua, Mhe. Gerald Mongella, akiambatana na baraza la madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kaliua, Mhe. Jafael Lufungija, Mkurugenzi Mtendaji, ndugu Jerry Daimon Mwaga, pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo, wamefanya ziara ya kujifunza mfumo wa stakabadhi ghalani katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa leo, Desemba 16, 2024.


Ziara hiyo imelenga kuboresha ufanisi wa ukusanyaji wa mazao na kuchochea ongezeko la mapato ya ndani kwa Wilaya ya Kaliua na wakulima wake.


Akizungumza katika ziara hiyo, Mhe. Mongella amesema, lengo kuu la ziara hiyo ni kuhakikisha kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani unaanzishwa na unatekelezwa kwa ufanisi katika Wilaya ya Kaliua ili kuboresha masilahi ya wakulima na kuongeza mapato ya Halmashauri. 


“Tumeamua kujifunza mfumo huu ili tufanye vizuri zaidi kwa masilahi ya wakulima wetu na mapato ya Kaliua,” ameisema Mongella.


Aidha, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kaliua, Mhe. Jafael Lufungija, ameshukuru kwa ukarimu wa Halmashauri ya Ruangwa na elimu waliyopata kuhusu mfumo huo. 


“Tumejifunza mengi na sasa kilichobaki ni kutekeleza kwa viwango vya juu hata zaidi ya mnavyofanya ninyi,” ameisema Lufungija.


Mbali na hayo. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ruangwa, Nolasco Kilumile, ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Kilimo na Mifugo, amesisitiza kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani ni mzuri na utasaidia kuongeza mapato kwa wakulima na Halmashauri kwa kutoa takwimu sahihi na kudhibiti wizi wa mazao. 


Ameongeza kuwa mfumo huo unawasaidia wakulima kuuza mazao yao kwa bei nzuri na fedha kuingia moja kwa moja kwenye akaunti za benki za wakulima.


Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ruangwa, Mhe. Andrew Chikongwe, amesema kuwa mfumo huo umeimarisha ukusanyaji wa mazao na mapato ya Halmashauri ya Ruangwa, akitoa mfano wa mazao makuu kama mbaazi, ufuta, na korosho. 


“Kaliua wakitekeleza mfumo huu, maisha yao yatabadilika kwa kiwango kikubwa,” ameisema Chikongwe.


Hata hivyo, Ziara hiyo pia imewanufaisha wageni hao kwa kutembelea miradi mingine muhimu wilayani Ruangwa, ikiwemo uwanja wa michezo wa Kassim Majaliwa na Shule ya Msingi Likangara iliyojengwa kwa kiwango cha ghorofa.


Ziara hiyo imekuwa fursa muhimu ya kubadilishana uzoefu na kuimarisha mifumo ya kiuchumi wilayani, huku ikilenga kukuza mapato ya ndani, maendeleo ya kilimo, na maisha ya wakulima.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa