• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Wakurugenzi Waagizwa Kusimamia Matumizi ya Fedha za Misitu.

Posted on: March 15th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Joseph Mkirikiti, amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Lindi kusimamia na kuhakikisha Maafisa Misitu wanaandaa mpango kazi na kuwasilisha taarifa ya matumizi ya fedha ambazo wamepokea na kuzifanyia kazi kutoka kwa Mfuko wa Misitu Tanzania( TaFF).

Mheshimiwa Mkirikiti amesema hatua hiyo itaziwezesha Halmashauri kurejeshewa fedha kwaajili ya utekelezaji wa shughuli za upandaji miti kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Mkuu huyo wa wilaya ya Ruangwa amesema hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bwana Godfrey Zambi alipomuwakilisha kwenye Maadhimisho ya Kampeni ya Upandaji Miti kimkoa yaliyofanyika Machi 15 katika shule ya sekondari Ruangwa wilayani hapo.

Mkuu wa Wilaya Mkirikiti amesema Fedha hizo zinazopaswa kurejeshwa katika Halmashauri ni zinazotoka na wafanyabiashara wa mazao ya misitu ambapo wanapaswa kulipa tozo ya asilimia 5 ya makusanyo kutoka misitu ya asili kwa ajili ya kugharamia shughuli ya upandaji miti Wilayani.

Ameongeza kuwa kwa mujibu wa muongozo huo wa uvunaji na biashara ya mazao ya misitu, tozo ya asilimia tano ya fedha za upandaji miti inatozwa kwenye mazao ya misitu kama vile kuni, mkaa, magogo, na nguzo.

“Kuna fedha ambazo zinapaswa kurudishwa katika halmashauri zetu kwaajili ya kuratibu shughuli hizi ila watu mnaohusika mnafanya uzembe wa kutokutekeleza majukumu yenu” amesema Mkirikiti

“Wakurugenzi msiwafumbie macho hawa watu wanaotaka kuturudisha nyuma, Kila mtumishi wa serikali azingatie majukumu yake na hakikisheni hizo fedha kwa Halmashauri ambazo hamjazipata watu wenu wawasilishe vitu vinavyotakiwa ili zipatikane” amesema Mkirikiti.

Aidha aliwataka wanafunzi kuwatayari kutunza mazingira yao kwa kupanda miti na kuitunza katika mazingira ya shuleni na hata majumbani kwani wao ndiyo mabalozi wanaotegemewa kuhakikisha mazingira yanakuwa mazuri.

“Miti tunayoipanda leo viongozi ni kwaajili ya taifa la kesho tunawapandia nyie hii miti mjitahidi kuitunza kwani mti inafaida nyingi mtakuwa na vivuli vya kutosha pale mnapohitaji kukaa nje ya madarasa” amesema Mkirikiti.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Christopher Ngubiagai ,amesema Kilwa ni Wilaya yenye misitu mingi na kuna vijiji vingi vinavyonufaika na misitu hiyo katika kuongeza kipato kwa mtu mmojammoja na Serikali ya kijiji.

Amesema Nanjilinji ni kijiji cha kwanza Kilwa kinachonufaika na utunzaji wa misitu kwani kupitia msitu wake wameishakusanya zaidi ya milioni 800 kwa miaka 5.

“Nanjilinji kupitia misitu wameweza kujenga ofisi nzuri na ya kisasa ya serikali ya kijiji, pia wamejenga nyumba ya kulala wageni na wamejiwekea utaratibu kila mwanafunzi wa darasa la saba anapofaulu kwenda sekondari wanatoa shilingi laki moja kumpa mtoto huyo’’amesemaNgubiagai

Ameongeza kuwa Nanjilinji mwanamke akipata  mimba anapewa shilling elfu 50 ya kitanzania kwa ajili ya kusaidia matunzo ya mimba  ambapo fedha hiyo inatokana na faida ya misitu waliyoihifadhi kijijini hapo.

Naye Mtendaji wa mradi Usimamizi Shirika rasimali za uvuvi Thomas Chale amesema shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF), watashirikiana na viongozi kuhakikisha mazingira ya Mkoa wa Lindi na Wilaya zake yanatunzwa kama inavyopaswa.

Mkoa wa Lindi umefanya maadhimisho ya siku ya upandaji miti kimkoa katika wilaya ya Ruangwa, huku kauli mbiu ikiwa ‘Tanzania ya Kijani Inawezekana Tupande Miti kwa Maendeleo ya Viwanda’.

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa