• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DC Ruangwa awataka watendaji kuchapa kazi

Posted on: December 22nd, 2018


Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mhe. Hashim Mgandilwa amewataka watendaji wote wa Kata na Vijiji waliopo Wilayani hapa kutatua kero za wananchi katika maeneo yao kabla wananchi awajaleta matatizo yao katika ofisi yake au Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwani wao ndio wakurugenzi katika maeneo yao.

Mhe. Mgandilwa amesema hayo alipokuwa kwenye kikao kazi alichokiitisha tarehe 22/12/2018 katika ukumbi wa CCM Ruangwa Mjini kwa ajili ya kutoa maelekezo mbalimbali kwa Watumishi na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.

Mhe. Mkuu wa Wilaya amewataka watendaji hao kujipangia ratiba na siku maalumu ya kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wananchi.

" Najua kuna baadhi ya watendaji hamkai katika maeneo yenu ya kazi, pangeni ratiba muiweke ofisini na muache namba za simu ili usipokuwepo mwananchi aweze kukutafuta kwa njia ya  simu"

"Inashangaza unaenda kwenye vijiji unakuta miradi ya maendeleo ila mtendaji wake ajui suala lolote la huo mradi, ni wajibu wenu kujua kila mradi unaoingia katika maeneo yenu" alisema

Wakati huo huo Mhe. Mgandilwa  amewataka watendaji wenye namba za simu za viongozi kutumia vizuri namba hizo na kuacha kupiga simu kwa viongozi bila utaratibu.

Amesema anajua kuna watendaji wananamba ya simu ya Waziri Mkuu niwatake muache mara moja tabia ya kumtafuta Mhe, Waziri kwani kuna  ofisi unayoweza kupeleka jambo lako hapa hapa Ruangwa na likatatuliwa.

"Ukija ofisini kwangu utaona kuna ofisi ya mbunge na kuna katibu wa Mbunge  na katibu wa Waziri Mkuu jimboni acheni kupiga piga simu zisizo na utaratibu huo siyo utaratibu " amesema Mgandilwa

Mhe. Mgandilwa ameitaka ofisi ya Utawala ya Wilaya kufuatilia vikao vya mapato na matumizi katika vijiji kama vinafanyika katika maeneo yao kwani ni wajibu wa wananchi kusomewa mapato na matumizi kila baada ya miez mitatu hata kama hakuna makusanyo ni lazima kikao kifanyike.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ngd. Andrea Chezue ametoa pongezi kwa watendaji kata na vijiji kwa kutimiza majukumu yao kama inavyotakiwa.

Ngd. Chezue  amewataka waendele kusimamia suala la ufaulu katika maeneo yao kama walivyofanya katika shule za msingi hadi Kupelekea Wilaya ya Ruangwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa na nafasi ya 84 kitaifa kati ya halmashauri 185.

Vile Vilevile amewataka watendaji hao kutatua changamoto za mipaka katika maeneo yao kabla ya kufika kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa  2019.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • TAARIFA KWA UMMA

    June 04, 2025
  • WANAFUNZI RUANGWA WAIBUKA KIDEDEA USAFI NA UNADHIFU UMISSETA 2025 MKOA WA LINDI

    June 01, 2025
  • MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA NISHATI SAFI WANDORWA

    May 28, 2025
  • RUANGWA YAPOKEA MWENGE WA UHURU 2025 KUTOKA LINDI MANISPAA

    May 28, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa