• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

DC RUANGWA AONGOZA UGAWAJI WA VITAMBULISHO KWA WAJASILIAMALI

Posted on: December 3rd, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, ameongoza zoezi la kugawa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo wadogo leo, Desemba 3, 2024, katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya, zoezi hilo limekusudia kuwatambua wajasiriamali wadogo wadogo na kurahisisha shughuli zao za kibiashara, huku likilenga pia kuepusha changamoto za ulipaji wa kodi zisizo za lazima.


Akizungumza wakati wa kugawa vitambulisho hivyo, Mhe. Ngoma amesisitiza kuwa vitambulisho hivyo ni kwa ajili ya wajasiriamali wadogo wadogo wanaozalisha chini ya shilingi milioni 4 kwa mwaka. Ameeleza kuwa dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuwezesha wajasiriamali wadogo wadogo kuendesha biashara zao bila usumbufu, na vitambulisho hivyo vinalipiwa  shilingi 20,000 tu kwa miaka mitatu.


“Mhe. Rais ametoa vitambulisho hivi kwa wajasiriamali wadogo wadogo wanaozalisha chini ya milioni 4 kwa mwaka, kama biashara yako inazalisha zaidi ya hapo, waachie wenye biashara ndogo ili nao wapate nafasi ya kujiinua,” amesema Mhe. Ngoma, huku akisisitiza umuhimu wa kuzingatia vigezo.


Hata hivyo, kati ya vitambulisho 307 vilivyopokelewa wilayani, ni 15 tu vilivyolipiwa na kugawiwa hadi sasa. Mhe. Ngoma amewahimiza viongozi wa maeneo mbalimbali kuhimiza wajasiriamali wadogo wadogo kulipia na kuchukua vitambulisho hivyo ili kurahisisha uendeshaji wa biashara zao. 


“Niwaombe viongozi kuwaelimisha wajasiriamali wadogo wadogo waliopo maeneo yenu juu ya umuhimu wa kulipia vitambulisho na kuvitumia kwa shughuli zao,” amesisitiza.


Kwa upande mwingine, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya, Ndugu Rashid Namkulala, amebainisha kuwa vitambulisho hivyo vinawahusu wajasiriamali wadogo wadogo kama mama lishe, baba lishe, bodaboda, machinga, na wauza mboga mboga. Hata hivyo, hadi sasa ni wajasiriamali wadogo wadogo 610 waliojisajili kwenye mfumo, kati yao ni 15 tu ndio waliolipia vitambulisho hali inayohitaji juhudi zaidi za kuwafikia walengwa.


Ikumbukwe kuwa vitambulisho hivi vinapaswa kuhuishwa kila baada ya miaka mitatu ili kuhakikisha vinabaki kuwa halali kwa matumizi ya kibiashara. Washiriki wa kikao hicho wameeleza matumaini makubwa ya kuona sekta ya biashara ndogo ndogo ikipata msukumo mpya kupitia mpango huu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa