• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM CHAENDELEA KUISAIDIA RUANGWA UWEKAJI WA MTANDAO WA ALAMA ZA UPIMAJI

Posted on: August 2nd, 2024

Timu ya wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia wakiongozwa na Mhadhiri Dkt. Joseph Mango, imefanya zoezi la kuweka mtandao mpya wa alama za upimaji na kisha kupima viwanja 90 katika Kijiji cha Mchangani, Kitongoji cha Maguja Wilaya ya Ruangwa, zoezi hilo ni sehemu ya mpango wa matumizi bora ya ardhi.


Timu hiyo yenye jumla ya watu 8, akiwemo Dkt. Alex Lubida, Dkt. Ijumulana Julian, Mr. Gideon Nchimbi, Ms. Sarah Muneja, Mr. Peter Barongo, Mr. Hassan Kihame na Mr. John Makuri, imeambatana na wanafunzi wa mwaka wa 2&3 wanaofanya mafunzo kwa vitendo (Field) kutoka chuoni hapo.


Kwa Pamoja, wameweka alama kuu saba za upimaji ardhi (control points) katika maeneo ya Mbekenyera Sekondari, Majaliwa Sekondari, Nangumbu “B” (Shule ya Msingi Ng’alile), Shule ya msingi Chingumbwa, Ruangwa/Maguja Sekondari, Mandalawe Sekondari na Liuguru Sekondari. Uwekaji wa alama hizi za msingi za upimaji una faida nyingi kwa Wilaya, ikiwemo kurahisisha upimaji wa viwanja na shughuli nyingine za upimaji.


Kwa upande mwingine, wataalamu hawa wamepima jumla ya viwanja 90 vya matumizi mbalimbali kama makazi na maeneo ya taasisi ikiwemo Ruangwa/Maguja sekondari. Wakati wakiendelea na zoezi la upimaji, walipata pia nafasi ya kuwaonesha wanafunzi vifaa vya upimaji ardhi. Pia walielezea namna vinavyoweza kufanya kazi. Kwa ujumla, yote yalifanywa na wataalamu hawa, yamefanyika kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwa, ikiongozwa na Mkurugenzi ndugu Frank Chonya.


Aidha, Mpima ardhi wa Wilaya ya Ruangwa, ndugu. Raymond Cholobi, amepongeza juhudi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika kusaidia Wilaya ya Ruangwa kwa kuweka mtandao wa alama za upimaji. "Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa msaada mkubwa walionyesha katika kutekeleza zoezi hili. Uwekaji wa mtandao huu ni hatua muhimu ambayo itarahisisha upimaji na matumizi bora ya ardhi katika Wilaya yetu tunathamini sana ushirikiano huu," amesema Cholobi.


Kwa upande wake, Kiongozi wa msafara huo, Dkt. Joseph Mango, ameonyesha kuridhishwa na utekelezaji wa zoezi hilo lenye manufaa makubwa kwa maendeleo ya jamii ya Ruangwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa