Kwa niaba ya Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Andrew Chikongwe ametumia kikao cha Baraza Maalum la kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutoa shukrani kwa viongozi mbalimbali walioshirikiana nao katika kipindi chao cha uongozi kinachotarajiwa kufikia ukomo Juni 20, 2025.
Katika hotuba yake, leo tarehe 17 Juni, 2025 Mhe. Chikongwe ametoa shukrani za pekee kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa, kwa uongozi wake thabiti na mchango mkubwa katika maendeleo ya Halmashauri ya Ruangwa. Lakini pia amemshukru Mhe Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu pesa nyingi zije kufanya maendeleo Ruangwa.
Aidha, ameeleza kuwa mafanikio yaliyopatikana yamechangiwa na ushirikiano wa karibu kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack; Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Ndugu Frank Fabian Chonya pamoja na Wakuu wa Idara na Watumishi wa Halmashauri hiyo.
Vilevile, amesisitiza kuwa mshikamano kati ya uongozi wa kisiasa na wataalamu umekuwa nguzo muhimu katika kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma bora kwa wananchi wa Ruangwa.
Kwa upande mwingine, Katibu Tawala wa Wilaya ya Ruangwa, Mhandisi Zuhura Rashid, ametumia nafasi hiyo kuwapongeza Waheshimiwa Madiwani kwa kumaliza kipindi chao cha uongozi salama na kuwatakia mafanikio mema katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.
Zaidi ya hayo, amebainisha kuwa ushirikiano uliokuwepo kati ya Madiwani na watendaji wa Halmashauri umechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya taasisi hiyo katika nyanja mbalimbali.
Ruangwa
Anuani ya Posta: S.L.P 51
Simu ya Mkononi: 0732932312
simu: 0732932312
Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa