• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

BMT YATOA MAFUNZO YA MICHEZO KWA WALIMU NA MAKOCHA WILAYANI RUANGWA

Posted on: December 16th, 2024

Baraza la Michezo la Taifa (BMT) leo tarehe 16 Desemba 2024, limeendesha mafunzo ya michezo kwa walimu wa michezo kutoka shule za msingi na sekondari pamoja na makocha wa vilabu mbalimbali vya michezo katika Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi.


Mafunzo hayo yameratibiwa kwa ushirikiano kati ya BMT na Ubalozi wa Ufaransa nchini Tanzania, huku yakitolewa na wataalam kutoka wizara husika ndani ya Baraza pamoja na wataalam wengine kutoka vyama mbalimbali vya michezo.


Aidha, Michezo inayohusika katika mafunzo hayo ni pamoja na mpira wa miguu, riadha, mpira wa kikapu, na mpira wa wavu.


Sambamba na hayo, mafunzo hayo yanatarajiwa kuinua viwango vya ufundishaji michezo kwa walimu na makocha, hatua itakayochochea maendeleo ya vipaji vya michezo mashuleni na ndani ya jamii.


Akizungumza kuhusu mafunzo hayo, Afisa michezo wa BMT Charles Maguzu  amesema lengo ni kuboresha uwezo wa walimu na makocha katika kuibua na kukuza vipaji vya wanafunzi na wachezaji wilayani humo.


“Tunataka kuona michezo inakuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya vijana na jamii kwa ujumla.”


Kwa upande mwingine, Mwl. Sifa Mwaya ambaye ni mshiriki wa mafunzo hayo ameeleza kufurahishwa na fursa hiyo, akisema itasaidia kuboresha mbinu zao za kufundisha na kuendesha michezo kwa weledi zaidi.


“Mafunzo haya ni fursa muhimu sana kwetu, natumini itakuwa hatua muhimu kwa ukuaji wa michezo shuleni na katika jamii.”


Baraza la Michezo la Taifa limeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi katika kuhakikisha maendeleo ya sekta ya michezo yanawafikia wananchi wa ngazi zote.

Matangazo

  • NAFASI ZA KUJITOLEA HALMSHAURI YA WILAYA YA RUANGWA February 13, 2026
  • FOMU YA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI February 02, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • ASHALONGO FC VS KIBWANA FARM FC, HAKUNA MBABE

    February 08, 2026
  • RAS LINDI AWAHIMIZA MAAFISA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO NA VYOMBO VYA HABARI

    February 05, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa