• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII RUANGWA WASAINI MIKATABA KUANZA KAZI RASMI

Posted on: September 1st, 2025

Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii 151 wa Wilaya ya Ruangwa wamesaini mikataba ya makubaliano ya utendaji kazi na Halmashauri leo tarehe 01 Septemba 2025, ikiwa ni hatua rasmi ya kuanza majukumu yao ya kazi.


Zoezi hilo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa na kuongozwa na Mwanasheria wa Halmashauri, Adv. Levina Mlelwa. Tukio hilo limeshuhudiwa pia na viongozi wa Idara ya afya, likiwa ni hatua muhimu ya kuanzisha rasmi ajira za wahudumu hao waliopatiwa mafunzo maalum ya huduma za afya ya jamii.


Aidha, akizungumza katika hafla hiyo, Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Feisal Said, amesisitiza kuwa mikataba hiyo ni alama ya kuanza rasmi majukumu ya wahudumu hao, ambapo wanapaswa kuzingatia maadili ya kazi. Amebainisha kuwa jukumu walilopewa si la kawaida bali ni dhamana kubwa inayohitaji bidii, kujituma na uadilifu katika kuwahudumia wananchi.


“Nendeni mkatekeleze majukumu yenu kwa weledi na uaminifu, kwa sababu wananchi wanatuhitaji na mafanikio yetu yatapimwa kwa utendajikazi eenu.” Amesema Dkt. Feisal.


Zaidi ya hayo, Dkt. Feisal amefafanua kuwa utendaji kazi wa wahudumu hao utapimwa kwa kuzingatia vigezo vya utendaji (key performance indicators), ambavyo ni sehemu ya mfumo wa kitaifa wa upimaji wa huduma za afya. Ameeleza kuwa vigezo hivyo vitawawezesha viongozi kutathmini ubora wa huduma zinazotolewa, ikiwemo ushirikiano na jamii, uwajibikaji na ufanisi katika kutekeleza majukumu ya kila siku.


Sambamba na hilo, Dkt. Feisal amesisitiza mshikamano na ushirikiano kati ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii na wataalamu walioko katika vituo vya afya na zahanati. Amesema ushirikiano huo utasaidia kuboresha taarifa za afya, kuongeza kasi ya rufaa kwa wagonjwa na kufanikisha kampeni za kitaifa za afya zinazotekelezwa katika ngazi ya jamii.


Vilevile, amewakumbusha wahudumu hao kufanya kazi kwa weledi na uaminifu, huku wakitekeleza jukumu la kuwafikia wananchi nyumba kwa nyumba. Ameongeza kuwa mtindo huo wa kazi unalenga kuhakikisha kila kaya inafikiwa na huduma za afya.


Kwa upande wao, baadhi ya wahudumu wa afya ngazi ya Jamii waliopata nafasi ya kuzungumza wameonesha furaha na shukrani kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kuwapatia mikataba yao. Wameahidi kuwa tayari kuanza kazi mara moja, kushirikiana na wananchi kwa ukaribu na kuchangia kwa vitendo katika kuimarisha huduma za afya kwa jamii ya Ruangwa.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKUU WA WILAYA YA RUANGWA AZINDUA ZOEZI LA UCHANJAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    September 02, 2025
  • WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII RUANGWA WASAINI MIKATABA KUANZA KAZI RASMI

    September 01, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI RUANGWA AMKABIDHI FOMU YA UTEUZI MGOMBEA WA CHAUMMA

    August 25, 2025
  • ELISHA AIPATIA RUANGWA NAFASI YA PILI UCHORAJI SHIMISEMITA 2025

    August 24, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa