• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

MKURUGENZI CHONYA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NAMBILANJE

Posted on: September 16th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Ndugu Frank Fabian Chonya, amekagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nambilanje leo tarehe 16 Septemba 2025, ziara hiyo inalenga kufuatilia kasi ya mradi na ubora wa miundombinu inayojengwa.


Katika ukaguzi huo, Mkurugenzi ameambatana na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Dkt. Feisal Said, ambapo wametembelea maeneo yote ya ujenzi. Mradi unatekelezwa kwa gharama ya shilingi milioni 613 na unajumuisha wodi za wagonjwa wa kulazwa, jengo la wazazi, huduma za wagonjwa wa nje (OPD), kichomea taka, sehemu ya kufulia pamoja na miundombinu ya maji safi na salama, hatua inayolenga kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa viwango bora.


Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Ndugu Chonya amesema ameridhishwa na kasi ya Mkandarasi na viwango vya ubora vinavyozingatiwa. 


“Nimefurahishwa sana na kasi ya Mkandarasi lakini pia ubora umezingatiwa kwa kiwango cha juu, niwaombe tu ujenzi ukamilike mapema ili wananchi wapate huduma bora kwa wakati,” amesema Chonya.

Aidha, Mkurugenzi amebainisha kuwa mradi wa Nambilanje ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati mpana wa Serikali wa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu na makazi yao. Ameongeza kuwa Serikali inahakikisha kila fedha inayotolewa kwa ajili ya miradi ya afya inatumika ipasavyo kwa manufaa ya wananchi.


Zaidi ya hayo, amewataka wananchi wa Nambilanje na Vijiji vya jirani kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri pamoja na Mkandarasi. Ametoa wito kwa wananchi kushiriki katika kulinda miundombinu ya kituo hicho na kuhakikisha kinawasaidia na kizazi kijacho.


Vilevile, Mkurugenzi amesisitiza kuwa mafanikio ya miradi kama hii yanahitaji mshikamano wa jamii na Serikali. Ameeleza kuwa huduma bora za afya hazipimwi tu kwa majengo mapya, bali pia kwa mshirikiano wa wananchi katika kudumisha usafi, kulinda vifaa na kuunga mkono mpango wa utoaji huduma bora.


Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Feisal Said, amesema kukamilika kwa kituo hicho kutapunguza changamoto za wananchi kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za afya. Ameeleza kuwa kituo kitakapokamilika kitatoa huduma muhimu za mama na mtoto, chanjo, matibabu ya dharura na magonjwa yasiyoambukiza, hatua ambayo itaongeza usalama wa jamii na kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • ZIMESALIA SIKU 16 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 13, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 18 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 11, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 23 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 06, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 24 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 05, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa