• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YATOA MAFUNZO YA SHERIA NA UTAWALA BORA RUANGWA

Posted on: March 7th, 2025


Wizara ya Katiba na Sheria imetoa mafunzo ya sheria, utawala bora, na haki za binadamu kwa Wakuu wa Idara, Vitengo, Kamati ya ulinzi na usalama na Watendaji wa Kata wa Wilaya ya Ruangwa, mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri leo, Machi 7, 2025.


Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha watumishi wa umma kuelewa misingi ya demokrasia, utawala bora, na haki za binadamu ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Mada zilizotolewa zimejikita katika utawala wa sheria, uwajibikaji, ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi, na umuhimu wa kuheshimu haki za binadamu katika utendaji wa kazi za Serikali.


Aidha, Mgeni rasmi katika mafunzo hayo amekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mhe. Hassan Ngoma, ambaye ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuandaa mafunzo hayo, amesema kuwa elimu hiyo itaongeza ufanisi kwa watumishi wa umma na kuboresha utendaji kazi ndani ya Wilaya ya Ruangwa.


“Tumeyapokea mafunzo haya kwa mikono miwili na tuko tayari kujifunza na tunaamini uelewa wetu katika utawala bora na haki za binadamu utaimarika, jambo ambalo litasaidia katika utoaji wa huduma kwa wananchi kwa uadilifu na haki,” amesema Mhe. Ngoma.


Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo, Ndugu Moses Mayombo ambaye ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu,  ameeleza kuwa mafunzo yamewapa mwanga kuhusu dhana ya utawala bora, umuhimu wa kufuata sheria, na namna ya kulinda haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yao. Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatasaidia kupunguza changamoto za kiutendaji zinazotokana na uelewa mdogo wa sheria na haki za wananchi.


Hapo awali, changamoto ya uelewa mdogo wa sheria, utawala bora, na haki za binadamu ilichangia matatizo katika utoaji wa huduma kwa wananchi, ikiwemo ucheleweshaji wa maamuzi na kutokuwepo kwa ushirikishwaji mzuri wa wananchi. Kupitia mafunzo hayo, watumishi wa umma wanatarajiwa kuwa na ufanisi zaidi, huku Serikali ikiendelea kutoa mafunzo zaidi ili kuhakikisha kila mtumishi anatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kwa kuheshimu haki za binadamu.


@katiba

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA RUANGWA AHIMIZA USAFI NA MAZOEZI KWA AJILI YA AFYA BORA

    May 10, 2025
  • SMAUJATA YAENDESHA ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WASICHANA RUANGWA

    May 09, 2025
  • BURIANI

    May 07, 2025
  • MHE. MAJALIWA AAINISHA MAFANIKIO MAKUBWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO RUANGWA CHINI YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

    May 03, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa