• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

Waziri Mkuu Akagua Mradi Wa Usambazaji Maji

Posted on: March 5th, 2018

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekagua mradi wa usambazaji maji kwenye vijiji vinavyopitiwa na mradi wa maji ya Mbwinji na ameridhishwa na unavyoendelea.

Mradi huo unaosimamiwa na mamlaka ya maji na Usafi wa Mazingira Masasi, Nachingwea(MANAWASA) unatarajiwa kukamilika machi 31,2018.

Waziri Mkuu alifanya ukaguzi huo alipofanya ziara yake ya kikazi Wilayani Ruangwa katika kioksi cha kuchotea maji kilichopo kwenye kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa.

“Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji” amesema Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema vijiji ambavyo vimenufaika na mradi huu Wilayani Ruangwa ni sita ambavyo ni Chiapi, Nandanga, Ipigo, Luchelegwa, Litama na Mbecha.

Amesema serikali ya awamu ya tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yote yenye tatizo hilo nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa MANAWASA Mhandisi David Mwamsojo alisema mradi huo utagharimu sh. Milioni 870.738 hadi kukamilika.

Amesema mradi huo unahusisha vijiji 12 vilivyo kwenye umbali wa kilomita tano kutoka kwenye bomba kuu pamoja na ujenzi wa vioski 18 vya kuchotea maji.

Mhandisi Mwamsojo amesema hadi sasa tayari kazi ya ulazaji mabomba na kuweka vituo 16 vya kuchotea maji katika vijiji 11 vinavyonufaika na mradi huo imekamilika na wananchi wanaendelea kupata huduma ya maji safi na salama.

Alitaja vijiji hivyo kuwa ni Mtepeche, Magereza, Mailisita, Mkotokuyana na Naipanga vya Wilaya na Nachingwea na Chiapi, Nandanga, Ipigo, Luchelegwa, Litama na Mbecha vya Wilaya ya Ruangwa

Matangazo

  • NAFASI ZA KUJITOLEA HALMSHAURI YA WILAYA YA RUANGWA February 13, 2026
  • FOMU YA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI February 02, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • ASHALONGO FC VS KIBWANA FARM FC, HAKUNA MBABE

    February 08, 2026
  • RAS LINDI AWAHIMIZA MAAFISA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO NA VYOMBO VYA HABARI

    February 05, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa