• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WATUMISHI WA AJIRA MPYA RUANGWA WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA e-Utendaji (WATUMISHI)

Posted on: February 12th, 2025

Watumishi wa ajira mpya katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa Watumishi Portal (e-Utendaji) unaowezesha usimamizi na upimaji wa utendaji wao wa kazi.


Mafunzo hayo yamefanyika Februari 12, 2025, yakiongozwa na Kinara wa Mfumo wa Watumishi Portal kwa Mkoa wa Lindi, Ndugu Mohamedi Hamisi Mohamedi, kwa kushirikiana na Maafisa Utumishi wa Wilaya, mfumo huo unalenga kurahisisha upimaji wa utendaji wa kazi kwa watumishi wa umma kwa kuhakikisha taarifa zao zinapatikana kwa urahisi na kwa uwazi.


Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu, Ndugu Frank Edger Komba, amesema mfumo huo ni muhimu katika kusimamia uwajibikaji wa watumishi. 


“Mfumo huu unatoa fursa ya kutathmini utendaji wenu kwa uwazi na kuhakikisha mnatekeleza majukumu yenu kwa weledi, ni muhimu kuutumia ipasavyo ili kuboresha huduma kwa wananchi,” amesema Ndugu Komba.


Kadhalika, Ndugu Mohamedi Hamisi Mohamedi ameongeza kuwa mfumo huo utarahisisha utendaji wa kazi kwa kuhakikisha kila mtumishi anajisajili na kurekodi shughuli zake za kila siku. 


“Watumishi wenzangu mnapaswa kuzingatia matumizi sahihi ya mfumo huu ili kurahisisha usimamizi wa rasilimali watu na kupima utendaji wanu kwa uwazi,” amesema Mohamedi.


Naye, Mmoja wa watumishi wapya Bi. Consolata Macha, ambaye ni mtendaji wa kijiji cha Lipande, amesema kuwa mfumo huu umemsaidia kuelewa jinsi ya kuweka taarifa zake za utendaji kazini. 


“Awali sikujua jinsi ya kuripoti kazi zangu kwa njia rasmi, lakini kupitia mafunzo haya nimejifunza namna mfumo unavyofanya kazi na umuhimu wake,” amesema Bi. Macha.


Hata hivyo ni muhimu kutambua kwamba, Kabla ya mfumo wa e-Utendaji, upimaji wa utendaji wa watumishi ulifanyika kwa njia za kawaida, jambo lililokuwa likisababisha ucheleweshaji wa tathmini, lakini kwa sasa mfumo huu unarahisisha upimaji wa utendaji kwa uwazi zaidi. Serikali inatarajia kuwa matumizi sahihi ya mfumo huu yataongeza uwajibikaji kwa watumishi wa umma na kuboresha utoaji wa huduma.

Matangazo

  • NAFASI ZA KUJITOLEA HALMSHAURI YA WILAYA YA RUANGWA February 13, 2026
  • FOMU YA USAJILI WA WAANDAAJI WA MAUDHUI MTANDAONI February 02, 2026
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • NGUVU YA HAZINA YA MADINI INAYOBADILI HATIMA YA WANARUANGWA

    February 11, 2026
  • ASHALONGO FC VS KIBWANA FARM FC, HAKUNA MBABE

    February 08, 2026
  • RAS LINDI AWAHIMIZA MAAFISA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO NA VYOMBO VYA HABARI

    February 05, 2026
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa