• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA RUANGWA WALA KIAPO

Posted on: August 4th, 2025

Jumla ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi 44 Jimboni Ruangwa wa ngazi ya kata wamekula viapo rasmi vya utii na kutunza siri, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Octoba 2025.


Hafla hiyo ya kiapo imefanyika leo tarehe 04 Agosti 2025 katika ukumbi wa Shule ya Wasichana Ruangwa, ikiongozwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa Mhe. Jonas Munguatosha Lyakundi, mbele ya wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Jimbo.


Katika kiapo hicho, wasimamizi hao wameapa kutekeleza majukumu yao kwa uaminifu, uadilifu na kwa kuzingatia sheria za nchi, kanuni za uchaguzi, pamoja na miongozo rasmi inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.


Aidha, kiapo cha kutunza siri kimelenga kuhakikisha kuwa wasimamizi hao hawatafichua taarifa au nyaraka zozote za uchaguzi bila idhini ya kisheria, hali inayolenga kulinda usalama wa taarifa na uhalali wa mchakato mzima wa uchaguzi.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mwl. Mbesigwe ambaye ni Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo amewataka wasimamizi hao kutambua uzito wa kiapo walichokula na kuwa waaminifu kwa taifa. 

“Mmekula kiapo mbele ya umma na mbele ya sheria sasa jukumu lenu ni kulinda imani ya wananchi na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa vitendo,” amesema Mwl. Mbesigwe.


Kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, kila msimamizi anapaswa kula kiapo rasmi cha fomu namba 6 na 7 kabla ya kuanza majukumu yake ili kuthibitisha dhamira ya kutekeleza wajibu kwa haki na bila upendeleo. Zoezi hilo ni sehemu muhimu ya kuhakikisha uwajibikaji na uwazi katika mchakato wa uchaguzi.


Wasimamizi hao 44 wanatarajiwa kusimamia shughuli zote za uchaguzi katika kata 22 za Jimbo la Ruangwa, ambapo kila kata itakuwa na wasimamizi wawili waliopata mafunzo na sasa wameshatimiza masharti ya kiapo cha kisheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA YAPATA USAJILI KWA MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA (CPD)

    November 20, 2025
  • MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

    November 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE KITAIFA 2025

    November 15, 2025
  • MAAFISA UTAMADUNI WAKUTANA NA WALAMBO, NGARIBA NA WAMILIKI WA VIWANJA VYA JANDO NA UNYAGO

    November 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa