• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

WASIMAMIZI WA VITUO RUANGWA WAAPISHWA, MBESIGWE AWATAKA KUZINGATIA UADILIFU

Posted on: October 26th, 2025

Wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura katika Jimbo la Ruangwa wameapishwa rasmi leo Oktoba 26, 2025, wakitakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu, uzalendo na kufuata sheria zote za uchaguzi.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa wasimamizi hao, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ruangwa, George Mbesigwe, amesema watendaji hao hawapaswi kuwa chanzo cha malalamiko bali wawe walinzi wa haki, amani na uhalali wa matokeo ya uchaguzi.


“Msimamizi wa kituo anatakiwa kuwa mfano wa uadilifu. Msikubali kuwa sababu ya malalamiko au vurugu. Fanyeni kazi kwa weledi, kwa kufuata sheria na taratibu zote za uchaguzi,” amesema Mbesigwe, akisisitiza umuhimu wa kutanguliza maslahi ya taifa mbele ya maslahi binafsi.


Aidha, Mbesigwe amesema wapiga kura wenye mahitaji maalum wanapaswa kupewa kipaumbele siku ya kupiga kura, Oktoba 29, 2025, ili kuhakikisha ushiriki wa makundi yote katika mchakato wa kidemokrasia.


Kwa upande mwingine, mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika Oktoba 26 na 27 yamegawanywa katika Tarafa tatu za Wilaya ya Ruangwa Tarafa ya Mnacho (Chuo cha VETA), Tarafa ya Ruangwa (Shule ya Sekondari ya Wasichana Ruangwa), na Tarafa ya Mandawa (Shule ya Sekondari Mbekenyera).


Vilevile, lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wasimamizi na wasaidizi wao ili kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu unafanyika kwa amani, uwazi na bila upendeleo, sambamba na kuhakikisha kila kura inahesabiwa kwa mujibu wa sheria.


Mbali na hilo, wasimamizi hao wameapishwa kwa kiapo cha kutunza siri na wamepatiwa mafunzo ya maadili ya kazi, huku wakitakiwa kutoa tamko la kujitoa au kutojihusisha na chama chochote cha siasa kabla ya kusimamia mchakato wa upigaji kura.


Kwa mujibu wa Mbesigwe, jumla ya wasimamizi na wasaidizi 1,211 watasimamia vituo 389 vilivyopo katika kata 22 za Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.


Sambamba na hayo, Mbesigwe amesema maandalizi hayo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha wananchi wa Ruangwa wanatekeleza haki yao ya kikatiba kwa amani na utulivu, huku akitoa wito kwa watendaji hao kulinda misingi ya haki, uadilifu na uwazi katika kila hatua ya mchakato wa uchaguzi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 17.11.2025 November 17, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA March 13, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI April 25, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III August 09, 2023
  • Ona zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA RUANGWA YAPATA USAJILI KWA MAFUNZO ENDELEVU YA KITAALUMA (CPD)

    November 20, 2025
  • MHE NGOMA AWAPONGEZA NMB KWA KUIPANDISHA THAMANI YA KOROSHO KWA WANANCHI WA RUANGWA

    November 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA LISHE KITAIFA 2025

    November 15, 2025
  • MAAFISA UTAMADUNI WAKUTANA NA WALAMBO, NGARIBA NA WAMILIKI WA VIWANJA VYA JANDO NA UNYAGO

    November 14, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa